Na WAMJW - DOM
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu leo amewaongoza Watumishi wa Wizara ya Afya katika zoezi la upandaji miti katika mji mpya wa Serikali ulio katika kata ya Mtumba, tarafa ya Kikombo Jijini Dodoma.
Katika zoezi hilo Waziri Ummy ameagiza Watumishi wote waliohusika katika upandaji wa miti hiyo kuhakikisha wanaitunza vizuri isitawi, na ameagiza kila mtu kuchukua jukumu hilo. "Hii miti ambayo tumeipanda sio tu miti ya kivuli na mapambo tu, bali imejumuisha miti ya matunda. Miti hii ambayo tunaipanda ili ikue na kustawi, lazima kila mtu, ambae amepanda mti wake kuhakikisha kwamba haufi" Alisema Waziri Ummy.
Mbali na hayo, Waziri Ummy amemwagiza Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Cheula kutenga maeneo kwa ajili ya Watumishi kufanya mazoezi ikiwa ni mpango wa Serikali ya awamu ya Tano kupambana na Magonjwa yasiyo yakuambukiza. "Mazingira ya hapa ni mazuri kweli kutembea, ukizunguka huu mji hukosi Kilomita 5, nitamwandikia Waziri Jenister atusaidie kuwa na mabafu kwa ajili ya watu wanaofanya mazoezi kubadilisha nguo jioni, ni lazima sehemu za kazi ziwe rafiki kwa watu kufanya mazoezi" alisema Waziri Ummy.
Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amempongeza Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula na kikundi chake kwa kuja na wazo la upandaji wa miti katika mji huo, na kuwa mfano wa kuigwa na Wizara nyingine. Katika zoezi hilo lililojumuisha viongozi mbalimbali wa wizara, jumla ya miti 470 imepandwa katika awamu ya kwanza, lengo ikiwa ni kupanda miti 525. Miti 320 iliyopandwa ni ya matunda, na mingine ni kwa ajili ya mapambo na kivuli.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
akijiandaa kupanda mti, wakati wa zoezi la upandaji miti katika
Mazingira ya jengo la Wizara ya Afya lililo katika mji wa Serikali
katika kata ya Mtumba jijini Dodoma.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
akimwagilia maji mti wake aliopanda, wakati wa zoezi la upandaji miti
lililo fanywa na Watumishi wa Wizara ya Afya katika mji wa Serikali ulio
kata ya Mtumba jijini Dodoma.
Katibu
Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Zainab Chaula akimwagilia maji mti alioupanda katika Mazingira ya Wizara
ya Afya, yaliyo katika Mji wa Serikali uliopo katika kata ya Mtumba
jijini Dodoma.
Mganga
Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akiweka mbolea katika mti
wake, katika Mazingira ya jengo la Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto lililo katika mji wa Serikali uliopo katika kata
ya Mtumba jijini Dodoma.
Katibu
Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Idara
Kuu ya Afya Dkt. Zainab Chaula (Wakatikati) akiteta jambo na Katibu
Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Idara
kuu Maendeleo ya Jamii Bw. Sebastian Kitiku (Wakulia) na Mganga Mkuu wa
Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi (Wakwanza kushoto)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu akifanya ukaguzi wa jengo la Wizara ya Afya lililo katika hatua
ya mwisho, leo wakati wa zoezi la upandaji miti katika Mazingira ya
jengo la Wizara ya Afya lililo katika mji wa Serikali katika kata ya
Mtumba jijini Dodoma.
Muonekano
wa jengo la Wazara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
lililo katika mji wa Serikali uliopo katika kata ya Mtumba jijini
Dodoma, jengo hilo liko katika hatua ya mwisho ya ujenzi
No comments:
Post a Comment