Takwimu
za vitendo vya ukatili kwa watoto nchini vinaonyesha kuwa mmoja kati
ya wasichana watatu na mmoja kati ya wavulana saba hufanyiwa ukatili wa
kingono kabla ya kufikisha miaka 18.
Alisema
hayo Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Watoto kutoka Wizara ya Afya Idara
Kuu Maendeleo ya Jamii anyeshughulikia masuala ya malezi kwa watoto na
familia Grace Mwangwa wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa Maafisa
Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Mikoa ya Shinyanga,
Katavi na Kigoma Mapema leo katika mji mdogo wa Kasulu Mkoani Kigoma.
Mafunzo
hayo kwa Maafisa hao yafanyika Mjini kasulu kwa lengo la kuwapatia
mafunzo ya Kitini cha Elimu ya Malezi ya Familia kwa Watoto na
kuwawezesha kupata mbinu na uwezo wa kuwajengea wazazi na walezi
maarifa na washiriki hao wanatoka kwenye Mikoa yenye kiwango kikubwa cha
mimba na ndoa za utotoni.
Aidha
Bi. Mwangwa aliwambia wajumbe wa mafunzo hayo kuwa viwango vya ukatili
wa kimwili ni asilimia 72 kwa wasichana na asilimia 71 ni wavulana
ambavyo vinasababishwa zaidi na wazazi, walezi wakiwemo walimu.
Bi.
Mwangwa alisema pia kuwa robo tatu ya watoto huadhirika zaidi na
ukatili wa kihisia kutokana na kutukanwa matusi, kubaguliwa na kupuuzwa
akiongeza kuwa Vitendo vyote hivi vinasababishwa na desturi na kanuni za
jamii zenye madhara na zinazounga mkono kutumia ukatili katika kumlea
mtoto.
‘’Ukosefu
wa uelewa, maarifa na stadi zinazohusu njia za malezi zisizo za ukatili
na umma kutoelimishwa vya kutosha kuhusu haki za mtoto pamoja na
umaskini wa kaya unaosababisha wazazi au walezi kuwatelekeza watoto,
uhamiaji kutoka vijijini kwenda mijini ambapo watoto hutolewa vijijini
na ndugu zao kwa ahadi za maisha mazuri na kudhoofika kwa mifumo ya
asili ya kijamii. Alisikika akisema Bi. Mwangwa.
Aliwaambia
washiriki wa kikao hicho kuwa nafahamu dhihiri kuwa,mfumo wa ulinzi wa
mtoto ni msingi imara ambao unapelekea uwekaji wa mazingira ya ulinzi
kwa watoto wetu kuanzia ngazi ya taifa,jamii na familia kwa ujumla.
Bi.
Mwangwa aliendelea kusema kuwa serikali kwa kushirikiana na wadau
imedhamiria kushughulikia ukatili dhidi ya watoto kwa kuweka sera,
sheria na mipango inayolenga kulinda haki za mtoto.
Kupitia
Kitini hiki cha Elimu ya Malezi ya Familia kwa Watoto washiriki
watapata mbinu na kuwa na uwezo wa kuwajengea wazazi/ walezi maarifa na
stadi juu ya mikakati ya kijamii ya kuzuia aina zote za ukatili dhidi
ya watoto kupitia elimu madhubuti ya malezi chanya yanayofaa katika
jamii.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Idara ya Watoto kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo
ya Jamii anyeshughulikia masuala ya malezi kwa watoto na familia Grace
Mwangwa pamoja na Kaimu Afisa Maendeleo wa Mkoa wa Kigoma Bw.
Msafiri Nzunuri wakifuatilia jambo wakati wa mafunzo kwa Maafisa
Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Mikoa ya Shinyanga,
Katavi na Kigoma Mapema leo katika mji mdogo wa Kasulu Mkoani Kigoma.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Idara ya Watoto kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo
ya Jamii anyeshughulikia masuala ya malezi kwa watoto na familia Grace
Mwangwa akitoa maelekezo wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa
Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Mikoa ya
Shinyanga, Katavi na Kigoma Mapema leo katika mji mdogo wa Kasulu Mkoani
Kigoma.
Afisa
Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya
Jamii anyeshughulikia masuala ya malezi kwa watoto na familia Bw.
Emmanuel Burton akitoa mada wakati wa mafunzo kwa Maafisa Maendeleo ya
Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Mikoa ya Shinyanga, Katavi na
Kigoma Mapema leo katika mji mdogo wa Kasulu Mkoani Kigoma.
Baadhi
ya Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Mikoa
ya Shinyanga, Katavi na Kigoma wakifuatilia kwa makini mafunzo ya Kitini
cha Elimu ya Malezi ya Familia kwa Watoto yanayotolewa na Wizara ya
Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii leo katika mji mdogo wa Kasulu.
No comments:
Post a Comment