SHIRIKA
la Railway Children limekutana na waandishi wa habari katika warsha
maalumu wa kutolea ufafanuzi kuhusu mazingira wanayoyapitia watoto
wanaoishi kwenye mazingira magumu pamoja na kutoa mafunzo kuhusiana na
uandishi wa habari za watoto yaliyofanyika leo katika hoteli ya New
Afrika jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa shirika hilo Mussa Mgata amesema kuwa watoto ni kundi muhimu ambalo linatakiwa kuangalia kwa ukaribu zaidi, na wao kama shirika wanaangalia kwa ukaribu zaidi kundi la watoto waishio kwenye maisha magumu pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili.
Mgata amesema kuwa mafunzo yaliyotolewa kwa wanahabari yatasaidia sana katika kujua matatizo yanayowakumba watoto katika mazingira yao na namna ya kuyatatua, amewataka wanahabari kutumia maarifa waliyoyapata katika kusaidia kuokoa kizazi hicho.
Kwa upande wake Meneja Miradi wa Shirika la Railway Children, Mary Gatama akitoa mada kuhusu watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wakati wa warsha hiyo amesema kuwa wao kama shirika watashirikiana na vyombo vya habari ambavyo huangaza jamii katika kuhakikisha changamoto zinazowakumba watoto zinapatiwa ufumbuzi.
Pia Afisa Mahusiano wa shirika hilo Henry Mazunda amesema kuwa suala la kuwalinda watoto ni jukumu la jamii nzima hivyo amewataka wanahabari kutumia kalamu zao vizuri katika kuonesha yale yanayowakumba watoto katika jamii.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa shirika hilo Mussa Mgata amesema kuwa watoto ni kundi muhimu ambalo linatakiwa kuangalia kwa ukaribu zaidi, na wao kama shirika wanaangalia kwa ukaribu zaidi kundi la watoto waishio kwenye maisha magumu pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili.
Mgata amesema kuwa mafunzo yaliyotolewa kwa wanahabari yatasaidia sana katika kujua matatizo yanayowakumba watoto katika mazingira yao na namna ya kuyatatua, amewataka wanahabari kutumia maarifa waliyoyapata katika kusaidia kuokoa kizazi hicho.
Kwa upande wake Meneja Miradi wa Shirika la Railway Children, Mary Gatama akitoa mada kuhusu watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wakati wa warsha hiyo amesema kuwa wao kama shirika watashirikiana na vyombo vya habari ambavyo huangaza jamii katika kuhakikisha changamoto zinazowakumba watoto zinapatiwa ufumbuzi.
Pia Afisa Mahusiano wa shirika hilo Henry Mazunda amesema kuwa suala la kuwalinda watoto ni jukumu la jamii nzima hivyo amewataka wanahabari kutumia kalamu zao vizuri katika kuonesha yale yanayowakumba watoto katika jamii.
Mkurugenzi
wa Shirika la Railway Children, Mussa Mgata akitolea ufafanuzi kuhusu
mazingira wanayoyapitia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wakati
wa warsha iliyowakutanisha waandishi wa katika mafunzo ya namna ya
kuandika habari za watoto yatakayofanyika leo katika hoteli ya New
Afrika jijini Dar es Salaam.
Meneja
Miradi wa Shirika la Railway Children, Mary Gatama akitoa mada kuhusu
watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wakati wa warsha
iliyowakutanisha waandishi wa katika mafunzo ya namna ya kuandika habari
za watoto yatakayofanyika leo katika hoteli ya New Afrika jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Mahusiano wa Shirika la Railway Children, Henry Mazunda akiwasilisha
mada ya namna kuwalinda watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu pamoja
na namna ya kutoa elimu ya jinsi ya kuwalinda watoto hao wakati wa
warsha ya iliyowakutanisha waandishi wa katika mafunzo ya namna ya
kuandika habari za watoto yatakayofanyika leo katika hoteli ya New
Afrika jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya waandishi wa habariwakiwa kwenye semina ya mafunzo ya namna ya
kuandika habari za watoto iliyoandaliwa na Shirika la Railway Children
iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka Blogu
ya Jamii
No comments:
Post a Comment