Serikali imesema inaunga mkono jitihada za Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk Reginald Mengi za kuanzisha nchini maabara ya kisasa ya kutumia tiba ya seli shina (Stem Cell), kwa madhumuni ya kutibu magonjwa mbalimbali yasiyo na tiba hadi sasa.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati akifungua kongamano la Kwanza la Kimataifa kuhusu tiba ya seli shina ( stem cells) kwa magonjwa ambayo hadi sasa hayana tiba.
Amesema licha ya kuwa Tanzania imeiboresha sana sekta ya afya kuna umuhimu jitihada hizo za serikali kuungwa mkono na wadau wa sekta binafsi.
Mapema akimkaribisha mgeni rasmi kufungua kongamano hilo Mwenyekiti Mtendaji wa IPP limited Dr Reginald Mengi amesema kusudio lake la kuanzisha maabara hiyo ya utafiti wa kisasa ni kutoa mchango wake katika kuiwezesha Tanzania kuwa na uwezo wa kutibu magonjwa ya binaadamu ambayo hayana tiba kwa sasa.
Aidha Mratibu Mipango wa Kampuni ya IPP Research, Technology and Innovation iliyoandaa kongamano hilo, Dr. Michael Magotti, na mwenzie Dr Kampon Sriwatanakul wamesema wanakusudia kuleta wazo jipya kuhusu tiba nchini na kwamba wameshapeleka maombi serikalini ya kuomba vibali vya kuanzisha maabara hiyo na lengo la kongamano hilo ni kuongeza uelewa kuhusu aina hiyo mpya ya matibabu kutoka kwa madaktari wabobezi kutoka nchi mbalimbali duniani.
Kongamano hilo limehudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya afya na tiba, huku kukiwa na mamilioni ya watu wenye ulemavu mbalimbali barani Afrika wakibaki majumbani kwao kwa kukosa uwezo wa kupelekwa India au nchi nyingine zilizoendelea ili kupatiwa matibabu.
Mwenyekiti
Mtendaji wa IPP limited Dr Reginald Mengi (kulia) akiongozana na Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine
Ndungulile (kushoto) kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano kwa ajili ya
kufungua kongamano la Kwanza la Kimataifa kuhusu tiba ya kutumia seli
shina (Stem Cell) kwa magonjwa ambayo hayana tiba, lililofanyika Hoteli
ya Serena jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni mstari wa nyuma
kutoka kushoto ni Mkuu wa Ubora wa Huduma Taasisi ya Moyo ya Jakaya
Kikwete (JKCI), Dr. Tulizo Sanga, Mratibu wa E-Medicine kutoka Idara ya
Tiba Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dr.
Liggy Vumilia pamoja na Mratibu Mipango wa Kampuni ya IPP Research,
Technology and Innovation iliyoandaa kongamano hilo, Dr. Michael
Magotti.
Mratibu
Mipango wa Kampuni ya IPP Research, Technology and Innovation
iliyoandaa kongamano hilo, Dr. Michael Magotti akitoa neno la ukaribisho
kwa mgeni rasmi na washiriki (hawapo pichani) wakati kongamano la
Kwanza la Kimataifa kuhusu tiba ya kutumia seli shina (Stem Cell) kwa
magonjwa ambayo hayana tiba, lililofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar
es Salaam.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine
Ndungulile akitoa hotuba ya ufunguzi wa kongamano la kwanza la
Kimataifa kuhusu tiba ya seli shina (Stem Cell) kwa magonjwa ambayo
hadi sasa hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research,
Technology and Innovation na kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini
Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa IPP limited Dr Reginald Mengi akizungumza dhumuni lake la
kuanzisha maabara ya kisasa ya tiba kwa kutumia seli shina (Stem Cell),
kwa madhumuni ya kutibu magonjwa mbalimbali yasiyo na tiba hadi sasa
wakati wa kongamano la kwanza la Kimataifa kuhusu tiba hiyo
lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research, Technology and Innovation na
kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Mishipa ya Fahamu ya Ubongo na Uti wa Mgongo kutoka
India, Prof. Alok Sharma (katikati) akimkabidhi Mwenyekiti Mtendaji wa
IPP limited Dr Reginald Mengi (wa pili kulia) zawadi ya kitabu
alichokiandika kuhusu matibabu ya kutumia seli shina (stem cell) kwa
magonjwa sugu yanayosababisha matatizo ya ubongo na mishipa ya fahamu
(Stem Cell Therapy in Neurological Disorders-4th Edition). Wanaoshuhudia
tukio hilo ni kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Stem Cell Afrika,
Andelene Thysse, Mratibu Mipango wa Kampuni ya IPP Research, Technology
and Innovation iliyoandaa kongamano hilo, Dr. Michael Magotti pamoja na
Dr. Kampon Sriwatanakul (kulia) kutoka Kampuni ya IPP Research,
Technology and Innovation.
Dkt.
Petcharin Srivatanakul kutoka Thailand akitoa mada kuhusu Uanzishwaji
wa maabara ya kutengeneza seli shina/chembechembe hai (Stem Cell) kwa
magongwa yasiyo na tiba wakati kongamano la Kwanza la Kimataifa kuhusu
tiba ya kutumia kinasaba cha kiinitete (Stem Cell) kwa magonjwa hayo
ambayo hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research, Technology
and Innovation na kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es
Salaam.
Dkt.
Daniel Maeda kutoka Idara ya Biolojia ya Molekyuli na Bayoteknojia,
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) akiwasilisha mada kuhusu “uwezo na
changamoto za seli shina za kiinitete na seli shina shawishi” wakati
kongamano la Kwanza la Kimataifa kuhusu tiba ya kutumia seli shina (Stem
Cell) kwa magonjwa hayo ambayo hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya
IPP Research, Technology and Innovation na kufanyika katika Hoteli ya
Serena jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa IPP limited Dr Reginald Mengi na ugeni wa wataalamu wa tiba
ya kutumia seli shina (Stem Cell) wakifuatilia mada mbalimbali
zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa kongamano la Kwanza la Kimataifa
kuhusu tiba ya kutumia seli shina (Stem Cell) kwa magonjwa hayo ambayo
hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research, Technology and
Innovation na kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Balozi
mstaafu Juma Mwapachu akiuliza swali wakati kongamano la Kwanza la
Kimataifa kuhusu tiba ya kutumia seli shina (Stem Cell) kwa magonjwa
hayo ambayo hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research,
Technology and Innovation na kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini
Dar es Salaam.
Baadhi
ya wadau mbalimbali wa sekta ya afya na tiba walioshiriki kongamano la
kwanza la Kimataifa kuhusu tiba ya seli shina (Stem Cell) kwa magonjwa
ambayo hadi sasa hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research,
Technology and Innovation na kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini
Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa IPP limited Dr Reginald Mengi (katikati) akibadilishana
mawazo na Daktari Bingwa wa masuala ya Ngozi kutoka Medical Tourism Fit
jijini Dallas-Marekani, Dr. Benedict Olusola (kushoto) pamoja na
Mkurugenzi Mtendaji wa IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha (kulia) wakati wa
kongamano la kwanza la Kimataifa kuhusu tiba ya seli shina (Stem Cell)
kwa magonjwa ambayo hadi sasa hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya
IPP Research, Technology and Innovation na kufanyika katika Hoteli ya
Serena jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa IPP limited Dr Reginald Mengi akimsalimia Binti mwenye
ulemavu uliotokana na ajali ya gari Wakonta Kapunda ambaye ni mshindi wa
wazo la kibiashara la shindano la kujenga hoja asili ya ujasiriamali
lililojulikana kama “DREAM TO GREATNESS“ lililoandaliwa wakati wa
uzinduzi wa kitabu cha “I Can, I Must, I Will-The Spirit of Success”
alipomwalika kushiriki kongamano la kwanza la Kimataifa kuhusu tiba ya
seli shina (Stem Cell) kwa magonjwa ambayo hadi sasa hayana tiba
lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research, Technology and Innovation na
kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Kulia kwa Dr
Mengi ni Mkurugenzi Mtendaji wa IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha.
Picha
ya pamoja ya washiriki wa kongamano la kwanza la Kimataifa kuhusu tiba
ya seli shina (Stem Cell) kwa magonjwa ambayo hadi sasa hayana tiba
lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research, Technology and Innovation na
kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa IPP limited Dr Reginald Mengi akimkabidhi Mkurugenzi wa
Stem Cell Afrika, Andelene Thysse (kulia) kitabu chake cha “I Can, I
Must, I Will-The Spirit of Success” wakati wa kongamano la kwanza la
Kimataifa kuhusu tiba ya seli shina (Stem Cell) kwa magonjwa ambayo hadi
sasa hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research, Technology
and Innovation na kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es
Salaam.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine
Ndungulile akiagana na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP limited Dr Reginald
Mengi (katikati) mara baada ya kufungua kongamano la kwanza la Kimataifa
kuhusu tiba ya seli shina (Stem Cell) kwa magonjwa ambayo hadi sasa
hayana tiba lililoandaliwa na Kampuni ya IPP Research, Technology and
Innovation na kufanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa IPP Touchmate, Bw.
Victor Tesha, Dr. Kampon Sriwatanakul (wa pili kulia) kutoka Kampuni ya
IPP Research, Technology and Innovation pamoja na Mratibu wa E-Medicine
kutoka Idara ya Tiba Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee
na Watoto, Dr. Liggy Vumilia (kulia).
No comments:
Post a Comment