HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 26, 2019

SEKTA ZA AFYA NCHINI ZA SHAURIWA KUITEKELEZA AFYA MOJA

Na OWM DODOMA.
Afya Moja ni dhana inayojumuisha sekta ya afya ya binadamu , wanyamapori, mifugo na  mazingira katika kujiandaa, kufuatilia  na kukabili magonjwa yanayoathiri binadamu ,wanyamapori na mifugo.

Kwa kutambua  umuhimu wa  Afya moja nchini, sekta za Afya zenye kujumuisha wataalam wa sekta ya Afya ya binadamu, Afya ya wanyamapori na mifugo pamoja na mazingira wametakiwa kuanza kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia dhana hiyo ili uimarishaji wa Afya ya binadamu uwe wa Ufanisi na matokeo bora.

Akiongea wakati wa warsha ya  maafisa viungo wa Afya moja kutoka Wizara, Idara, Taasisi,  Mashirika ya serikali na ya Kimataifa, mjini Morogoro leo tarehe 26, Februari, 2019, Mkurugenzi Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Matamwe Jimmy, amefafanua kuwa tayari wataalamu hao wanao Mkakati wa kuzileta pamoja  Sekta za Afya kwa ajili ya kuzuia, kukinga na kuthibiti madhara na magonjwa yanayoikumba nchi yetu, yaani magonjwa ambukizi kati ya wanyama na binadamu pamoja na usugu wa vimelea vya magonjwa hivyo ni wakati wa kutekeleza mkakati huo kwa  kuitumia dhana ya Afya moja.

“Ninaamini kwamba, wote mnafahamu kuhusu tishio kubwa la magonjwa kama vile homa ya bonde la ufa, kwenye nchi za Afrika Mashariki , virusi vya Ebola Afrika Magharibi, kusambaa kwa kiasi kikubwa cha ugonjwa wa mafua ndege, (HPAI), matatizo ya kupumua yanayosababishwa na virusi vya Corona, mlipuko wa homa ya Lassa huko Africa Magharibi na homa ya Zika huko Amerika ya Kusini, kwa hiyo mifano michache magonjwa hayo yamekuwa tishio kubwa kwa afya ya binadamu na wanyama duniani kote.” Amesisitiza Kanali Matamwe.

Wakiongea wakati wa warsha hiyo wataalamu wa sekta za Afya hizo wamebainisha kuwa tayari wamekubaliana mfumo wa kutoa taarifa na kuhuisha utekelezaji wa mpango mkakati wa afya moja nchini.

Tarehe 13 Februari 2018, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa alizindua Dawati la Uratibu la Afya moja chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, likiwa na lengo la kusimamia na kuratibu shughui za Afya moja nchini. Kwa kutambua umuhimu huo  Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, kupitia Dawati la Uratibu wa Afya moja  kwa kushirikiana na USAID na   Chemonics International wameandaa mkutano wataalam hao.
 Mkurugenzi Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe akieleza  jambo wakati  wa warsha ya  maafisa viungo wa Afya moja mjini Morogoro leo tarehe 26, Februari, 2019.
 Mtaalamu wa Afya moja toka sekta ya Afya ya Mifugo, Dkt. Joseph Masambu akichangia juu ya  umuhimu wa dhana ya Afya moja nchini wakati  wa warsha ya  maafisa viungo wa Afya moja mjini Morogoro leo tarehe 26, Februari, 2019.
 Baadhi ya Wataalamu wa sekta za Afya , sekta ya Afya ya binadamu, Afya ya wanyamapori na mifugo pamoja na mazingira  wakifuatilia  warsha ya  maafisa viungo wa Afya moja mjini Morogoro leo tarehe 26, Februari, 2019.
 Mtaalamu wa Afya moja toka sekta ya Afya ya Binadamu, Profesa. Japhet kilewo akichangia juu ya  umuhimu wa dhana ya Afya moja nchini wakati  wa warsha ya  maafisa viungo wa Afya moja mjini Morogoro leo tarehe 26, Februari, 2019.
Maafisa viungo wa Afya moja kutoka Wizara, Idara, Taasisi,  Mashirika ya serikali na ya Kimataifa, wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa warsha ya Uongozi wa  maafisa viungo wa Afya moja mjini Morogoro leo tarehe 26, Februari, 2019.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad