Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametuma
salamu za rambirambi kwa familia zilizopoteza jamaa zao katika ajali ya barabarani iliyotokea katika Wilaya
ya Mbozi Mkoani Songwe na kusababisha vifo vya watu 19.
Ajali
hiyo imetokea jana tarehe 21 Februari, 2019 majira ya saa 3:15 usiku katika
mteremko wa mlima Senjele ambapo lori (Semi-trailer)
lililokuwa likisafiri kutoka Tunduma kwenda Mbeya Mjini lililigonga basi la
abiria kwa nyuma, kisha basi hilo likaminywa katikati baada ya kuligonga lori
jingine (Semi-trailer)
lililokuwa mbele yake na kusababisha
vifo vya watu wote 18 waliokuwemo ndani ya basi pamoja na dereva wa lori lililogonga basi la abiria.
Mhe.
Rais Magufuli amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig.
Jen. Mstaafu Nicodemas Elias Mwangela kufikisha
salamu zake za pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na vifo vya
watu hao na amewaombea kwa Mwenyezi Mungu aziweke roho za Marehemu wote mahali
pema peponi, Amina.
Aidha,
Mhe. Rais Magufuli amezitaka mamlaka zinazohusika na usalama wa barabarani
Mkoani Songwe kufanya uchunguzi wa ajali hiyo na kuchukua hatua zinazostahili
pamoja na kujipanga vizuri kukabiliana na matukio ya ajali za barabarani.
Wakati huo huo,
Mhe. Rais Magufuli ametoa mkono wa pole kwa familia
ya Waziri wa Maliasili na Utalii
Dkt. Hamisi Kigwangalla ambaye amefiwa na mwanae aitwaye Zul Hamis Kigwangalla
jana tarehe 21 Februari, 2019 Jijini Dar es Salaam.
Mhe.
Rais Magufuli akiwa na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli wamefika nyumbani kwa
familia hiyo Mikocheni Jijini Dar es Salaam na kukutana na baadhi ya
wanafamilia wakiongozwa na Mama wa Marehemu Dkt. Bayoum Kigwangalla wakiwa
katika maandalizi ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Nzega Mkoani Tabora.
Dkt. Hamis Kigwangalla ameshatangulia
Nzega ambako mazishi yatafanyika baadaye leo.
Gerson
Msigwa
Mkurugenzi
wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar
es Salaam
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisaini
kitabu cha Maombolezo, Victoria Jijini Dar es salaam nyumbani kwa Waziri wa
Maliasili na Utalii Dkt. Hamis Kigwangala, kufuatia kifo cha Mtoto wake aitwaye
Zul Hamis Kigwangala Kilichotokea Februari 21,2019 katika Hospitali ya Taasisi
ya Moyo ya Jakaya Kikwete (Muhimbili) Jijini
Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mkono wa pole na Dkt. Bayoum Kigwangala ( Mke wa Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Kigwangala), pamoja na Bi Hawa Mushi na Bi. Bagaile Bakari nyumbani kwa Waziri huyo Victoria Jijini Dar es salaam, kufuatia kifo cha Mtoto wake aitwaye Zul Hamis Kigwangala Kilichotokea Februari 21,2019 katika Hospitali ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (Muhimbili) Jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Watoto Hk Junior ,Sheila na Hawa ambao ni watoto wa Waziri wa
Maliasili na Utalii Dkt. Hamis Kigwangala alipoambata na mkewe Mama Janeth
Magufuli kutoa pole kwa Familia ya Waziri huyo nyumbani kwake Victoria Jijini
Dar es salaam, kufuatia kifo cha Mtoto wake aitwaye Zul Hamis Kigwangala
Kilichotokea Februari 21,2019 katika Hospitali ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya
Kikwete (Muhimbili) Jijini Dar es
Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
katika Dua maalum na mkewe Mama Janeth Magufuli ,Dkt. Bayoum Kigwangala (Mke wa
Dkt. Kigwangala), Hk Junior , Sheila, Hawa (Watoto wa Waziri Kigwangwala)
pamoja na Bi Hawa Mushi na Bi. Bagaile Bakari nyumbani kwa Waziri huyo Victoria
Jijini Dar es salaam, kufuatia kifo cha Mtoto wake aitwaye Zul Hamis Kigwangala
Kilichotokea Februari 21,2019 katika Hospitali ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya
Kikwete (Muhimbili) Jijini Dar es
Salaam
No comments:
Post a Comment