HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 5, 2019

MTIBWA WAENDELEA KUJINOA KUWASUBIRI AFRICAN LYON IJUMAA HII



Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
TIMU ya Mtibwa Sugar kinashuka dimbani siku ya Ijumaa ya tarehe katika mchezo wake wa  ligi kuu bara (TPL) dhidi ya African Lyon.


Mchezo huo utachezwa katika uwanja wa nyumbani wa Mtibwa Sugar (Manungu) unatarajiwa kuwa wa ushindani kwa pande zote mbili..


Kuelekea mchezo huo Msemaji wa klabu hiyo Thobias Kifaru na kusema kuwa maandalizi kwa kikosi kizima yanaendelea vizuri na wachezaji wana hari ya kuhakikisha wanabakisha alama tatu katika Uwanja wa nyumbani.

‘sisi kama wenyeji kila kitu kinaenda vizuri katika maandalizi ya mchezo huo, kilichobaki ni mchezo wenyewe na tunawaomba wana mtibwa ,wana Morogoro na wapenzi wetru waje kwa wingi watupe support,” Kifaru

Tunaamini African Lyon ni timu nzuri lakini hatutawabeza kabisa na hatutaki kupoteza mchezo huo muhimu kwetu.


Kikosi cha Mtibwa Sugar kitaendelea kukosa huduma ya Kelvin Sabato na Dickson Job ambao wako katika majaribio, Sabato yuko Afrika Kusini katika klabu ya Tshakuma Tsha Madzivhandila na Dickson Job yeye yupo katika majaribio Arsenal Kiev.

Lakini kikosi cha wana tam tam kimezidi kuimarika kutokana na wachezaji waliokosekana katika michezo iliyopita kurejea ambao ni Salum Kihimbwa alikuwa anatumikia kadi nyekundu, Juma Luizio na Jaffari Kibaya pia wamerejea katika kikosi baada ya kuwa wamepewa mapumziko.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad