HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, January 21, 2019

Wakazi wa Dar es Salaam wanufaika na Promosheni ya Tusua Ada na Omo

Meneja wa Game Supermakert ya Mlimani City, Josephat Okumu (kushoto), akimkabidhi mshindi wa droo ya pili, Grace Mboka mkazi wa Goba jijini Dar es Salaam pesa taslimu Shilingi laki tano(500,000/=) aliyoshinda katika Promosheni ya “Tusua Ada na Omo” inayoendelea.Dro hiyo iliyochezeshwa mwishoni mwa wiki katika Supermarket hiyo.Katikati ni Meneja wa Omo, Upendo Mkusa.
Meneja msaidizi wa Coppies Supermaket ya Mlimani City Edger Matilya(kulia), akimkabidhi mshindi wa droo ya pili, Shidu Abubakari mkazi wa Tegeta Dawasco jijini Dar es Salaam pesa taslimu Shilingi laki tano(500,000/=) aliyoshinda katika Promosheni ya “Tusua Ada na Omo” inayoendelea.Dro hiyo iliyochezeshwa mwishoni mwa wiki katika Supermarket hiyo.Katikati ni Meneja wa Omo, Upendo Mkusa.


WAKAZI sita wa jiji la Dar es Salaam wafanyao manunuzi katika Supermarket za Game,Choppies Mlimani City na Shoppers Mikocheni,Masaki na Mbezi wamejishindia jumla ya shilingi milioni tatu(3,000 000) ikiwa ni shilingi laki tano(500,000/=) kila mmoja baada ya droo ya pili kufanyika mwishoni mwa wiki. Washindi hao walipatikana mara baada ya kununua Omo na kuingia rasmi kwenye droo kubwa inayochezeshwa katika Supermakert kila jumamosi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Meneja wa Omo, Upendo Mkusa kwanza aliwapongeza washindi wote haswa watatu waliopatikana katika droo ya pili kukamilisha idadi ya washindi sita ambao ni Grace Mboka mkazi wa Goba aliyeshinda katika Supermaket ya Game Mlimani City, Shidu Abubakari alishinda katika Supermaket ya Choppies Mlimani City na Lilian Patrick aliyeshinda katika Supermakert ya Shoppers ambapo aliwaomba pesa walizoshinda wakazielekeze kwenye elimu kwa watoto wao kama kauli mbio ya kampeni inavyo sema “Tusua Ada na Omo”.

Kampuni ya Unilever kupitia bidhaa yake ya Sabuni ya Omo wanatambua kama jamii ya Watanzania imetoka katika kipindi cha Siku kuu ya Chrismass na Mwaka mpya hivyo wakaona ni jambo jema kuungana na wanafamilia katika kipindi hiki cha watoto kwenda shule kuchangia kwa namna moja ama nyingine kupitia promosheni hii.

Alisema Upendo, katika Promosheni hii ya Tusua Ada na Omo jumla ya Shilingi milioni sita (6,000 000/=) zitatolewa kwa washindi 12 ikiwa kila mmoja atajishindia pesa taslimu Shilingi laki tano(500,000/=).

Alisema Upendu ushiriki uko wazi kwa kila mtu lakini lazima uwe na umri zaidi ya miaka 18, ni lazima ununue Omo 1kg moja ziwe pakti mbili au 500gm pakti ziwe nne au 3.5kg pakti moja,ambapo mshiriki utapewa kuponi ya itakayoingizwa kwenye droo itakayochezesha kila jumamosi ya juma hilo.

Mwisho Upendo aliwaomba wakazi wa jiji la Dar es Salaam kuchangamkia fursa ya pesa hiyo kwani ushiriki na ushindi wake uko wazi. Nikufanya manunuzi ya Omo katika Supermakert ya Game,Choppies au Shoppers Mikocheni, Msaki au Mbezi tayari unaweza kujishindia pesa taslimu Shilingi 500,000/=.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad