Meneja wa Game Supermakert ya Mlimani City,
Josephat Okumu (kushoto), akimkabidhi mshindi wa
droo ya pili, Grace Mboka mkazi wa Goba jijini Dar
es Salaam pesa taslimu Shilingi laki tano(500,000/=)
aliyoshinda katika Promosheni ya “Tusua Ada na
Omo” inayoendelea.Dro hiyo iliyochezeshwa
mwishoni mwa wiki katika Supermarket
hiyo.Katikati ni Meneja wa Omo, Upendo Mkusa.
Meneja msaidizi wa Coppies Supermaket ya
Mlimani City Edger Matilya(kulia), akimkabidhi
mshindi wa droo ya pili, Shidu Abubakari mkazi wa
Tegeta Dawasco jijini Dar es Salaam pesa taslimu
Shilingi laki tano(500,000/=) aliyoshinda katika
Promosheni ya “Tusua Ada na Omo”
inayoendelea.Dro hiyo iliyochezeshwa mwishoni
mwa wiki katika Supermarket hiyo.Katikati ni
Meneja wa Omo, Upendo Mkusa.
WAKAZI sita wa jiji la Dar es Salaam wafanyao
manunuzi katika Supermarket za Game,Choppies
Mlimani City na Shoppers Mikocheni,Masaki na
Mbezi wamejishindia jumla ya shilingi milioni
tatu(3,000 000) ikiwa ni shilingi laki tano(500,000/=)
kila mmoja baada ya droo ya pili kufanyika
mwishoni mwa wiki. Washindi hao walipatikana mara baada ya kununua
Omo na kuingia rasmi kwenye droo kubwa
inayochezeshwa katika Supermakert kila jumamosi.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Meneja wa
Omo, Upendo Mkusa kwanza aliwapongeza
washindi wote haswa watatu waliopatikana katika
droo ya pili kukamilisha idadi ya washindi sita
ambao ni Grace Mboka mkazi wa Goba aliyeshinda
katika Supermaket ya Game Mlimani City, Shidu
Abubakari alishinda katika Supermaket ya Choppies
Mlimani City na Lilian Patrick aliyeshinda katika
Supermakert ya Shoppers ambapo aliwaomba pesa
walizoshinda wakazielekeze kwenye elimu kwa
watoto wao kama kauli mbio ya kampeni inavyo
sema “Tusua Ada na Omo”.
Kampuni ya Unilever kupitia bidhaa yake ya Sabuni
ya Omo wanatambua kama jamii ya Watanzania
imetoka katika kipindi cha Siku kuu ya Chrismass na
Mwaka mpya hivyo wakaona ni jambo jema
kuungana na wanafamilia katika kipindi hiki cha
watoto kwenda shule kuchangia kwa namna moja
ama nyingine kupitia promosheni hii.
Alisema Upendo, katika Promosheni hii ya Tusua
Ada na Omo jumla ya Shilingi milioni sita
(6,000 000/=) zitatolewa kwa washindi 12 ikiwa kila
mmoja atajishindia pesa taslimu Shilingi laki
tano(500,000/=).
Alisema Upendu ushiriki uko wazi kwa kila mtu
lakini lazima uwe na umri zaidi ya miaka 18, ni
lazima ununue Omo 1kg moja ziwe pakti mbili au
500gm pakti ziwe nne au 3.5kg pakti moja,ambapo
mshiriki utapewa kuponi ya itakayoingizwa kwenye
droo itakayochezesha kila jumamosi ya juma hilo.
Mwisho Upendo aliwaomba wakazi wa jiji la Dar es
Salaam kuchangamkia fursa ya pesa hiyo kwani
ushiriki na ushindi wake uko wazi. Nikufanya manunuzi ya Omo katika Supermakert ya
Game,Choppies au Shoppers Mikocheni, Msaki au
Mbezi tayari unaweza kujishindia pesa taslimu
Shilingi 500,000/=.
No comments:
Post a Comment