HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, January 4, 2019

UYUI KUJENGA DAHARIA(HOSTEL) 15 ZENYE THAMANI YA BILIONI 1.5 KUWALINDA WANAFUNZI WA KIKE

NA TIGANYA VINCENT, TABORA
SERIKALI Wilayani Uyui imesema inakusudia kuendesha Kampeni maalumu ya Nishike Mkono Mwezi Machi mwaka huu kwa lengo la kukusanya shilingi bilioni 1.5 (1,500,000,000/-) ambazo zitasaidia ujenzi wa dahari(hosteli) 15 kwenye Sekondari 15 za Kata ili kuwalinda watoto wa kike na mimba na ndoa za utotoni.

Kauli hiyo imetolewana Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa mama wadogo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tabora-Uyui yaliandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuwajengea uwezo watoto wa kike ambao walikubwa na tatizo la mimba za utotoni.

Alisema lengo la kujenga daharia hizo ni kuwaepusha wanafunzi wa kike wa shule za Sekondari na mimba, vishawishi vinavyowafanya washindwe kuendelea na shule na kuozeshwa na wazazi wao , kuwapa utulivu wa kujisomea kwa kuwa karibu na mazingira ya shule na kuwaepusha kuacha shule kwa sababu ya kutembea umbali mrefu wa kwenda shule ambapo wakati mwingine wanakutana na matatizo ya kutaka kubakwa.

Mkuu huyo wa Wilaya hiyo alisema kuwa kukamilika kwa Daharia hizo sio tu kutasaidia watoto wa Kata husika bali wale wanaotoka Kata jirani ambazo hazina Sekondari ambapo wanafunzi wao wanatembelea umbali mrefu kwenda jirani.

Aidha Msuya alisema mafunzo hayo ni muhimu sana kwa vijana ili wapate elimu kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo malezi na familia, afya ya lishe , ujasirimali, kilimo biashara , uongozi , taratibu za uundwaji wa vikundi vya uzalishaji mali na fursa za uwezeshaji wa vijana kiuchumi.

Aliwataka mama wadogo hao kutumia fursa waliyopata ya kupata mafunzo ili kujiendeleza wenyewe na kueneza elimu waliyopata kwa mama wadogo ambao hawakupata ya kupata elimu hiyo. Msuya alitaja Kata ambapo daharia zitakazojengwa ni Magiri , Igalula, Goweko, Usagari, Ilolanguru, Lutende, Mabama, Shitage, Upuge, Ikongoro, Makazi, Tura , Isikizya na Loya.

Naye  Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Julius Toneshi alisema mafunzo hayo ni kitaifa ambayo yanalenga kuwawezesha mama wadogo kupata mbinu na stadi za kujitambua, uthubutu, kufanya maamuzi sahihi na kujiwekea malengo katika maisha yao.

Alisema programu hii inalenga katika kuboresha ustawi na maendeleo kwa mama wadogo kwa kuwapatia fursa za uwezeshaji kiuchumi. Naye Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Tabora Baraka Makona alisema jumla ya mama wadogo 90 kutoka mkoani humo watapata mafunzo hayo ambapo 45 wanatoka Uyui na Kaliua 45.

Alisema wameamua kuanzia Wilaya hizo kwa sababu ndizo zinaongoza kwa mimba na ndoa za utotoni. Mafunzo hayo yanaendeshwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Halmashauri za Wilaya ya Tabora -Uyui na Kaliua 
  Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Tabora Baraka Makona akitoa maelezo mafupi mafunzo mafupi kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyojenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea 
malengo katika maisha yao.
  Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Julius Toneshi akitoa maelezo mafupi mafunzo mafupi  kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyojenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.
 Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya akifungua  mafunzo mafupi  kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyolenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.
 Baadhi ya mama wadogo wakiwa katika mafunzo ya siku mbili mafunzo yalilenga kuwajenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.
 Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na mama wadogo  mara baada kufungua  mafunzo mafupi  kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyolenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.
  Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya (mwenye miwani) akibadilishana mawazo na mama wadogo mara baada kufungua  mafunzo mafupi  kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyolenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.
Mkuu wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya (mwenye miwani ) akiwa amebeba mtoto mara baada kufungua  mafunzo mafupi  kwa mama wadogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora yaliyolenga kuwajengea uwezo wa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi ya kujiwekea malengo katika maisha yao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad