HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, January 28, 2019

Taasisi ya Dk Ntuyabaliwe yakabidhi maktaba Tandale Magharibi

Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi amezindua Maktaba ya Shule ya Msingi Tandale Magharibi na kutoa wito kwa wanafunzi kuitumia vyema maktaba hiyo kujenga maarifa.
Aidha amewataka wanafunzi kuilinda maktaba hiyo kama chanzo cha maarifa na weledi.
Maktaba hiyo imewezeshwa na taasisi hiyo kufuatia shindano la Andika Chalenge kwa shule za serikali nchini.
Aliwataka pia wazazi kutekeleza jukumu lao la kushawishi watoto kusoma vitabu na kutumia maktaba na kuwa weledi katika masomo kwa kujisomea.
Akizindua maktaba hiyo ambayo Taasisi iliikarabati, kuweka mashubaka pamoja na vitabu vya aina mbalimbali, Mwenyekiti wa Taasisi, Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi amesema amejisikia furaha kutimiza ahadi ya kukabidhi maktaba kwa shule hiyo iliyotoa mshindi.
Katika  shindano hilo la uandishi la Andika Challenge ambalo linafanyika mikoa yote Tanzania na kushirikisha wanafunzi wote wa shule za msingi za serikali kuanzia darasa la 4 mpaka la 7 ambapo wanafunzi huandika hadithi na kutuma kwa sanduku la posta 163 Dar es salaam, washindi huzawadiwa tuzo na shule aliyotoka husaidiwa kuwa na maktaba.
Shule ya Msingi Tandale Magharibi imepata maktaba hiyo baada ya mwanafunzi wake Nuurat Venance kushinda shindano la kutunga hadithi lililowashindanisha wanafunzi wa shule za msingi za manispaa za Kinondoni na Ubungo, jijini Dar es salaam.  Hivi sasa shindano hilo linawashindanisha wanafunzi  wote wa shule za msingi hapa nchini.
Alisema baada ya mshindi kupatikana mwaka jana ambaye alitoka katika shule hiyo, taasisi ilibaki na changamoto ya kuwezesha kupatikana kwa maktaba, na anapoifungua maktaba hiyo anafurahishwa kuwa taasisi imetekeleza ahadi yake kwa mshindi wa shindano hilo.
Jacqueline Mengi akizungumza katika makabidhiano hayo alisema kwamba nia kubwa wa shindano hilo ni kusaidia watoto kujua kusoma na kuandika na pia kuwa wabunifu na kutumia ubunifu wao kusonga mbele.
Alisema pamoja na serikali kuwezesha elimu bure, wao kama taasisi wanatoa mchango wao ambao utasaidia kuimarishwa kwa tabia ya kusoma na kujipatia maarifa kutoka katika maktaba.
Alisema taasisi ya Dk Ntuyabaliwe iliyoanzishwa kwa ajili ya kumuenzi baba yake ambaye alikuwa anapenda sana kujisomea vitabu na kuwahimiza watoto wake akiwemo yeye kujifunza kusoma,  kwa sasa inaendesha shindano hilo la Andika Challenge ili kuhakikisha kwamba wanafunzi wanajijenga katika ubunifu na matumizi wa lugha ya Kiswahili kwa kutunga hadithi zao wenyewe.

Anasema kwa msimu huu mashindano hayo yanaendelea na kwamba vigezo vinavyostahili kufanywa na wanafunzi kuanzia darasa la 4 hadi la 7.
Ikiamini kwamba kusoma na kuandika ndio njia pekee ya kukabiliana na wanafunzi wanaomaliza shule bila kujua kuandika Jacquline alisema kwa sasa wamewezesha shule 7 kuwa na maktaba, wanafunzi 4,406 kusaidia mambo mbalimbali na vitabu takaribani 20,827 kuwafikia wanafunzi.
Mapema Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Grace Mtesigwa alisema kitendo cha kukabidhi maktaba kwa shule hiyo, Taasisi ya Dk Mtuyabaliwe imekuwa ikiunga mkono kwa vitendo jitihada za Rais John Magufuli za kuboresha elimu nchini.
Wakitoa shukrani kwa niaba ya shule, Mwalimu Mkuu Doris Msigalo na Mwakilishi wa Wazazi  Sudi Makamba wameishukuru Taasisi na kusisitiza kuwa wataitumia na kuitunza vizuri maktaba hiyo.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akisalimiana na Mwakilishi wa Wazazi na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa,  Sudi Makamba mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Shule ya Msingi Tandale Magharibi kwa ajili ya tukio la kuzindua maktaba mwishoni mwa juma jijini Dar es Salaam.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Tandale Magharibi mara baada ya kuwasili shuleni hapo kwa ajili ya tukio la kuzindua maktaba lililofanyika mwishoni mwa juma jijini Dar es Salaam.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akiuliza maswali kwa wanafunzi wa shule ya msingi Tandale Magharibi mara baada ya kuwasili shuleni hapo kwa ajili ya tukio la kuzindua maktaba lililofanyika mwishoni mwa juma jijini Dar es Salaam.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akiimba pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Tandale Magharibi mara baada ya kuwasili shuleni hapo kwa ajili ya tukio la kuzindua maktaba  lililofanyika mwishoni mwa juma jijini Dar es Salaam.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Tandale Magharibi mara baada ya kuwasili shuleni hapo kwa ajili ya tukio la kuzindua maktaba  lililofanyika mwishoni mwa juma jijini Dar es Salaam.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akikata utepe kufungua maktaba mpya ya shule ya msingi Tandale Magharibi iliyojengwa na taasisi hiyo jijini Dar es Salaam katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa juma. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mwalimu Mkuu  wa shule hiyo, Doris Msigalo (katikati), Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Grace Mtesigwa (wa kwanza kulia) pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akikata utepe kufungua maktaba mpya ya shule ya msingi Tandale Magharibi iliyojengwa na taasisi hiyo katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa juma. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Grace Mtesigwa, Mwakilishi wa Wazazi  Sudi Makamba, viongozi wa bodi ya shule pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Grace Mtesigwa wakipitia baadhi ya vitabu vilivyotolewa na taasisi hiyo kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya msingi Tandale Magharibi kujisomea na kuongeza maarifa.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akimkabidhi moja ya kitabu mwanafunzi  Nuurat Venance aliyeshinda shindano la kutunga hadithi “Andika Challenge” lililowashindanisha wanafunzi wa shule za msingi za manispaa za Kinondoni na Ubungo, jijini Dar es salaam na kupelekea shule yake kujengewa maktaba na taasisi hiyo.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akipewa mkono wa pongezi na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Grace Mtesigwa mara baada ya kuonyesha picha za muonekano wa jengo la maktaba ya shule ya msingi Tandale Magharibi lilivyokuwa awali.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi akimkumbatia mwanafunzi  Nuurat Venance aliyeshinda shindano la kutunga hadithi “Andika Challenge” lililowashindanisha wanafunzi wa shule za msingi za manispaa za Kinondoni na Ubungo, jijini Dar es salaam na kupelekea shule yake kujengewa maktaba na taasisi hiyo.
 Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Tandale Magharibi, Doris Msigalo akitoa neno la shukrani Muasisi na mwenyekiti wa taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi mara baada ya kuwakabidhi jengo jipya la maktaba shuleni hapo.
Muasisi na mwenyekiti wa  taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi  katika picha ya pamoja na uongozi wa Shule ya msingi Tandale Magharibi na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo mara baada ya kufungua maktaba mpya iliyojengwa na taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Muasisi na mwenyekiti wa taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi  akisalimiana na Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandrah aliyemwakilisha mtoto wake aliyesoma shule ya msingi Tandale Magharibi kushiriki halfa ya uzinduzi wa maktaba mpya shuleni hapo.Katikati ni Dj wa Diamond Platnumz Romy Jones.
Muasisi na mwenyekiti wa taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi  katika picha ya pamoja na Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandrah (wa pili kulia), Dj wa Diamond Platnumz Romy Jones (wa pili kushoto), Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Grace Mtesigwa (kulia) pamoja na dada wa Diamond Patnumz, Esma Platnumz.
Baadhi ya walimu wa Shule ya Msingi Tandale Magharibi wakipiga ‘Selfie’ na Muasisi na mwenyekiti wa taasisi ya Dk Ntuyabaliwe, Jacqueline Mengi  mara baada ya kufungua maktaba mpya shuleni hapo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad