HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, December 19, 2018

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB achaguliwa kuwa mwenyekiti wa umoja wa Mabenki Tanzania

Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernerd Kibese (wa pili kulia) akimpongeza Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Mabenki Tanzania ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela baada ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo, jana kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Umoja huo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartted , Sunjay Rughani, na wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania, Tusekelege Mwaikasu-Jounde.
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernerd Kibese akifurahi jambo na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartted , Sunjay Rughani. Katikati ni Mwenyekiti Mpya wa Umoja huo ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela 
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernerd Kibese akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wanachama wa Umoja wa Mabenki Tanzania, baada ya kikao chao kilichofanyika jana kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. Katika kikao hicho kulifanyika uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu wake ambapo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela aliibuka mshindi na kuchukua kijiti cha Mwenyekiti wa Umoja huo, huku nafasi ya Makamu ikichukuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartted , Sunjay Rughani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad