Na.Khadija seif,globu ya jamii
KATIKA
kusherehekea siku yake ya kuzaliwa Msanii wa filamu nchini Irene
Uwoya amefanya dua ya Kuwarehemu watu maarufu waliotangulia mbele ya
haki.
Akizungumza
wakati wa kutoa neno la shukrani kwa watu ambao wamejumuika nae kwenye
sherehe hiyo ikiwemo watu wenye ulemavu na wasiojiweza Irene amesema
amefanya hivyo ili kurudisha fadhila kwa watu ambao siku zote wamekua
wakitazama kazi zake pamoja na kununua .
Uwoya
ameeleza kuwa ni muhimu kuwasaidia watu wasiojiweza na kuwapatia
mahitaji ili waweze kujisikia faraja na kuona wasanii wapo pamoja nao na
kwa Leo ameweza Kula nao chakula pamoja na kuwapatia zawadi. "Hakuna
kitu kikubwa kama fungu la Kumi kwani sio hiyari na mafanikio yangu ni
kutokana na kutoa sadaka kwa wingi hakuna uchawi wowote bali ni kufanya
sadaka kwa wingi na kumuomba mwenyezi mungu "alisema Irene uwoya
Kwa
upande wa Mlezi wa kituo kinachowalea watoto yatima Almadina center
kilichopo Tandale Yusra Mohamed ametoa pongezi kwa Irene Uwoya kwa
kuwafariji watoto hao pamoja na walemavu kwani ni wasichana wachache
wenye maono kama yake kuwapa nafasi watu hao kujumuika nao pamoja .
Hata hivyo watoto wameshukru na kufurahi siku ya Leo japo imekua ni mara chache kupatiwa misaada na kusubiri siku za sikukuu. Watoto
Hawa ni wa kwetu sote tuwasaidie na kushirikiana nao katika kuwalea na
kuwakuza katika maadili mema na yanayompendeza mwenyezi mungu.
Pia
kwa upande wa Kiongozi wa Wasanii wa filamu ambae pia ni mtu wa karibu
wa Irene uwoya, Steve Nyerere amempongeza Irene kwa kujumuika na watu
hao na kuwashauri wasanii wengine waige mfano na kuwaenzi na kuwaombea
dua kwa wingi watu waliofanya mazuri hapa nchini .
No comments:
Post a Comment