HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 30, 2018

YANGA YAJIKITA KILELENI BAADA YA USHINDI WA 3-0 DHIDI YA JKT TANZANIA

Na Agness Francis, blogu ya Jamii. 
VIJANA wa Jangwani Yanga SC wameibuka na ushindi baada ya kuwatandika mafande wa JKT mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa leo katika dimba la Taifa Jijini Dar es  Ligi Kuu Tanzania Bara(TPL). 

Yanga anakaa kileleni kwa kufikisha alama 35 wakiwa na  michezo 13 wakishinda mechi kumi na sare mbili, ambapo Azam akiwa chini yao kwa pointi  33 michezo  sawa na Yanga, huku Simba akiwa nafasi ya tatu alama 27. 

Mtanange huo wa aina yake ulioanza majira ya saa kumi jioni na kila upande  walicheza kwa kukamiana na  kutafuta magoli ya ushindi ambapo kwa kipindi hicho cha kwanza na katika  dakika  ya 19 za mapema Yanga anapata bao la ushindi kutoka kwa mchezaji Heritier Makambo kutikisa nyavu za JKT ambapo anafikia rekodi ya mchezaji wa Simba Meddie 8 Kagere kwa kufikisha idadi ya  magoli 7.

Mpira uliendelea kupigwa kila timu ilishambulia lango la Maafande wa JKT wakitafuta goli la kusawazisha na Yanga wakitafuta magoli ya kuongoza mpaka wachezaji wanaenda mapumzikoni matokeo yalibaki kuwa ni 1-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi zaidi  kwa pande zote JKT walionyesha kufika langoni kwa Yanga ambapo wamelenga mashuti yasio Leta madhara kwa Yanga, na dakika ya  52 mchezaji Mrisho  Ngasa (Anko) ameiandikia klabu yake goli 2.

Mchezo uliendelea kuchezwa kwa kuwakamiana JKT wwalionyesha kushambulia langoni kwa Yanga kutafuta magoli wakati Yanga waliitaji ushindi zaidi wa magoli mengi na kutoka na alama ili kujiweka Katika msimamo wa nafasi nzuri Ligi kuu Tanzania bara (TPL). 

Katika dakika za 78  Ibrahim Ajibu anaiandikia timu yake goli la 3 kwa mkwaju wa Penati iliyosababishwa na mchezaji wa JKT kuunawa mpira, 

Kocha mkuu wa klabu ya  yanga Mwinyi Zakhera amezungumza na waandishi  wa habari ni baada ya dakika 90 za mchezo kumalizika kati uwanja wa Taifa amesema kuwa "Nimefurahishwa na matokeo wachezaji wangu wamejitahidi licha ya  jana saa nne usiku kupigiwa simu kuwa  tff wamebadilisha ratiba muda wa kuchezwa mechi ambapo ilitakiwa ichezwe saa 12 jioni, na kusema itachezwa sa 10 jioni"

Zahera amesema "lakini haikuwa sawa ilitakiwa watoe taarifa masaa 24 kabla"

Huku kocha mkuu wa JKT Bakari Shime amesema kuwa  "tulipata nafasi nne mpaka tumeshindwa kuzitumia inamana tungezitumia vema tungekuwa na matokeo mazuri, baada ya goli la 2 wachezaji wangu walionyesha kukosa kujiamini, mimi kama kocha nitakaa na wachezaji wangu na kufanyia kazi makosa yetu"

Mchezo ujao Yanga anatarajia kusafiri mkoani Mbeya kumenyana na Prison katika uwanja wa Sokoine Disemba 3.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad