HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 29, 2018

KAZI INAKWENDA VIZURI MRADI WA RELI YA KISASA KUTOKA DAR MPAKA SINGIDA MAKUTUPORA


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii, Dodoma
Kazi inakwenda vizuri. Ndivyo unavyoweza sema kuhusu mradi wa reli ya kisasa marufu ya Standard Gauge kutokana na Shirika la Reli(TRC) kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa ikiwemo kumsimamia mkandarasi Yepi Merkezi kwa ukaribu mkubwa.

Michuzi Blog imetembelea mradi huo, kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora, ambako kuna vipande viwili vya mradi huo vinavyotekelezwa na mkandarasi huyo, kujionea kuna mabadiliko makubwa  kuhusu ujenzi huo tofauti na watu wanavyozungumza katika Mitandao ya Kijamii na Vijiweni.

Hii inatokana na kuwepo kwa madai ya kuwa hakuna kazi inayofanyika, ambapo iko wazi kabisa kuwa kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro kazi imefanyika kwa zaidi ya asilimia 36, ambapo sehemu zilizobakia ni ndogo na zinazoweza kufanyiwa kazi kwa uharaka na mkandarasi.

Pia, inaelezwa hata baadhi ya malighafi nyingi zinapatikana kwenye eneo la mradi iwe kipande cha Morogoro hadi Makutupora au Dar es Salaam hadi Morogoro, ambapo imerahisisha upatikanaji wa marighafi.

Akizungumza na Michuzi Blog Meneja mradi wa SGR kwa upande wa Shirika la Reli nchini(TRC), Injinia Masanja Machibya, amesema hakuna malighafi yeyote inayozalishwa nje, bali mahitaji yote muhimu yanapatikana kwenye eneo la mradi.

Meneja mradi wa SGR kwa upande wa Shirika la Reli nchini(TRC), Injinia Masanja Machibya, akizungumza na Waandishi wa habari  kuhusu mradi huo unavyoendelea katika Lot 1 inayotoka Dar es Salaam mpaka Morogoro.
Meneja mradi wa SGR kwa upande wa Shirika la Reli nchini (TRC), Injinia Masanja Machibya,akiwaonesha Wanndishi wa Habari mfano wa Reli ya SGR itakavyokuwa katika kiwanda cha kuzalisha Mataluma ya Reli hiyo.
Mafundi Wakiendelea na Ujenzi wa Madaraja na karavati katika eneo la mradi wa SGR eneo la Lot 1 Kisarawe.

Mataluma ya Reli yakiwa yameweka kwa ajili ya kutandikwa juu ili kujenga mradi wa SGR kwa upande wa Shirika la Reli nchini(TRC),
Sehemu ya Wakandarasi wakiendelea na upandaji nyasi kwa ajili ya kuzuia Mmomonyoko wa udongo  kwenye tuta la kukatisha reli ya SGR.
Mafundi chuma wa mradi wa SGR Kutoka Yap Markenz wakiendelea na kazi ya kujenga Madaraja ya kupachika katika yard ya Shaurimoyo Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad