HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, October 22, 2018

WAZIRI WA UJENZI, MHANDISI KAMWELE AKAGUA UJENZI BARABARA SITA DAR-KIBAHA


Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Injinia Patrick Mfugale (kulia) akimwelezea Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Issack Kamwele (katikati) maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara sita kutoka Dar es Salaam hadi Maili Moja Kibaha unaojengwa na fedha za Serikali kwa gharama ya takribani zaidi ya shilingi bilioni 140. Waziri Mhandisi Kamwele alitembelea kukagua maendeleo ya mradi huo na miradi mingine ya Tanroads iliyopo jijini Dar es Salaam. Mradi wa ujenzi wa barabara sita unatarajiwa kukamilika mwezi wa kwanza 2020.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Injinia Patrick Mfugale (kushoto) akimwelezea Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Issack Kamwele (kulia) maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara sita kutoka Dar es Salaam hadi Maili Moja Kibaha unaojengwa na fedha za Serikali kwa gharama ya takribani zaidi ya shilingi bilioni 140.

Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Julius Ndyamukama (aliye nyoosha kidole) akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Issack Kamwele alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara sita kutokea Dar es Salaam hadi Mail Moja Kibaha.
  
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe pamoja na msafara wake wakitembelea mradi wa barabara sita unaoendelea eneo la Kimara Dar es Salaam hadi Mail Moja Mkoa wa Pwani.

Ujenzi wa barabara sita kutokea Dar es Salaam hadi Mail Moja Kibaha ukiendelea. Eneo hili unajengwa ukuta kuzuia maji ya mto kuingilia barabara hizo.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe akipata maelekezo ya ujenzi wa barabara sita kutoka kwa wataalam wa Tanroads.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza na wananchi akiwa katika ziara ya kukagua ujenzi wa barabara sita kutokea Dar es Salaam hadi Mail Moja Kibaha. Katika ziara hiyo Waziri Kamwelwe aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Rais John Pombe Magufuli katika jitihada za kumaliza msongamano wa magari kuingia na kutoka Dar es Salaam.  

Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe aalipozungumza nao katika ziara ya kukagua ujenzi wa barabara sita kutokea Dar es Salaam hadi Mail Moja Kibaha.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza na wananchi akiwa katika ziara ya kukagua ujenzi wa barabara sita kutokea Dar es Salaam hadi Mail Moja Kibaha. Katika ziara hiyo Waziri Kamwelwe aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Rais John Pombe Magufuli katika jitihada za kumaliza msongamano wa magari kuingia na kutoka Dar es Salaam.  

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya MECCO, Abdukadri Budjet (wa kwanza kushoto) mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Mbezi-Goba-Wazo Hill yenye urefu wa kilometa 5 inayojengwa na kampuni ya MECCO.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza na wanahabari mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Mbezi-Goba-Wazo Hill yenye urefu wa kilometa 5.

Muonekano wa kivuko cha waenda kwa miguu eneo la njia panda Kawe kituo cha Bondeni jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Injinia Patrick Mfugale (katikati) akifafanua jambo kwa  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Issack Kamwele (wa pili kushoto) alipokagua maendeleo ya daraja la Mlalakuwa jijini Dar es Salaam, linalojengwa na Serikali kwa takribani ya shilingi bilioni 4.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (kulia) akitoa maelekezo kwa wahandisi wa kampuni ya KIKA (kulia) wanaojenga Daraja la Mlalakuwa eneo la JKT jijini Dar es Salaam alipokagua mradi huo.

Sehemu ya ujenzi wa Daraja la Mlalakuwa eneo la JKT jijini Dar es Salaam ukiendelea.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad