HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 10, 2018

WAFANYAKAZI BENKI YA TIB CORPORATE WAMTEMBELEA MKURUGENZI WA TTCL

WAFANYAKAZI benki ya TIB Corporate leo wamemtembelea mteja wake ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba.

Wafanyakazi hao wamemtembelea kwajili ya kujitathmini juu ya huduma zao katika wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila ifikapo Oktoba kila mwaka.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba akizungumza na MICHUZI BLOG amewashukuru benki ya TIB kwa kufanya kazi kwa ufanisi pamoja na uaminifu.

Pia amewapongeza kwa kufika ofisini kwake na ka kufanya kazi kwa vitendo sio kukaa ofisini na kuwashukuru wateja wake.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba akizungumza na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo na kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya benki hiyo.
Mfanyakazi wa benki ya TIB Corporate, Grace Wilbard akimpa ua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba wakati alipotembelewa na wafanyakazi wa wa benki ya Tib Corporate jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni njia moja wapo ya kusheherekea wiki ya huduma kwa mtaja ambayo hufanyika kila oktoba.

Mkurugenzi wa idara ya sheria benki ya TIB Corporate Edward Lyimo  akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya biashara wa benki ya TIB Corporate Mwallu Mwachin'ga Kushoto ni Mkurugenzi idara ya uendeshaji wa benki ya TIB Corporate.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba jijini Dar es Salaam leo walipomtembelea ofisini kwake ikiwa ni kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad