HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 13, 2018

UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA LIWALE NA KATA 37 ZA TANZANIA BARA WAFANYIKA LEO

Wananchi wa jimbo la Liwale wamepongezwa kwa kujitokeza kwa wingi na mapema kwenda kupiga kura kuwachagua viongozi wanaowataka, 

 Hayo yameelezwa na Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Balozi Ramadhani Mapuli akiwa anafuatili uchaguzi mdogo katika Jimbo la Liwale. 
Balozi Mapuli amesema kwamba, ameridhishwa na utaratibu wa upigaji wa kura ikiwa ni pamoja na vituo kufunguliwa kwa wakati na hakuna malalamiko yoyote yaliyojitokeza katika hatua za awali. 

 Amewasihi wakazi wa Jimbo hilo kuendelea kujitokeza kwa wingi na kupiga kura katika hali ya amani na utulivu.
Kwa mujibu wa Mkurugezi wa uchaguziJimbo la Liwale  Luiza Mlelwa amesema  kuwa Jimbo hilo lina wapiga kura  55,777 na Vituo vya kupigia kura 158. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad