Kwa kipindi hiki ambacho tunahitaji kuelekea katika sera ya uchumi wa viwanda Tanzania inahitaji jamii iliyo
huru, yenye demokrasia na inayofuata haki katika juhudi zake za kuwaleletea
maendeleo wananchi wake.
Hayo
yameelezwa jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for
Civil Society Bw. Francis Kiwanga wakati akipokea Ruzuku ya shilingi billion
14.3 za kitanzania ambayo ni sawa dola za kimarekani milioni 6.25 kutoka katika Ubalozi wa Sweden wa hapa Tanzania kwa ajili ya kuwezesha kazi za Asasi za
Kiraia (AZAKI).
Ruzuku hiyo
itatumika katika kujenga demokrasia na utawala bora kwa kuboresha AZAKI,
kuongeza ushawishi na ushiriki wa wananchi katika maswala ya sera za maendeleo
pamoja na mafunzo kwa kipindi 2018 – 2020.
Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Bw. Francis Kiwanga akisaini hati ya kupokea msaada wa zaidi ya bilion 14 za kitanzania kutoka Ubalozi wa Sweden hapa nchini kwa ajili za kuwezesha Asasi za Kiraia.
Makubaliano
hayo yamefanyika jana oktoba 5, 2018 katika ubalozi wa Sweden hapa nchini
Tanzania uliopo posta jijini Dar es salaam na kutiwa saini na Balozi wa Sweden nchini
Bw. Anders Sjoberg pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Bw. Francis Kiwanga.
Akiongea
baada ya zoezi la kusaini Ruzuku hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation For Civil Society Bw. Francis
Kiwanga amesema kuwa Taasisi hiyo imejikita katika kuwasaidia watanzania na
imeweka nguvu kubwa katika kuimiza uwajibikaji na utawala bora pamoja na
kuwajengea uwezo vijana, wanawake na makundi mengine ili kusaidia
maendeleo yao na ya nchi kwa ujumla.
“Sekta ya Asasi za Kiraia (AZAKI) nchini sasa ni jukwaa madhubuti la kuhabarisha, kuwezesha
na kuhamasisha wananchi kufuatilia,kuhoji na kushiriki katika jitihada za
serikali katika ngazi zote. Ruzuku hii kwa kiwango kikubwa sana itatuongezea
nguvu katika kufanikisha hilo”. amesema Bw. Kiwanga
Balozi wa Sweden nchini Bw. Anders Sjoberg akisaini mkataba na Taasisi ya FCS wa kusaidia AZAKI za hapa nchini, mkataba huo uliosainiwa jana katika ubalozi wa Sweden hapa Tanzania.
Ameongeza
kuwa kwa miaka 16 sasa uwezeshaji wa FCS kwa azaki umefikia wilaya zote za
Tanzania bara na Zanzibar, kupitia utoaji Ruzuku na huduma za kujenga uwezo kwa
Asasi zaidi ya 5000, Na nyingi ni za ngazi ya chini na katika jamii zilizopo
vijijini.
Kwa upande
wake balozi wa Sweden nchini Bw. Anders Sjoberg alisema kuwa Sweden imeamua
kushirikiana na Foundation for Civil Society kutokana na uwezo pamoja na
kujituma kwake katika kuwezesha sekta ya asasi za kiraia ili kushiriki
kikamilifu katika kujenga utawala bora nchini Tanzania.
“Kuwezesha asasi za kiraia kunatoa
nafasi ya kujenga uwajibikaji na uwazi katika jamii” alisema Balozi Sjoberg
Balozi wa Sweden nchini Bw. Anders Sjoberg akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Bw. Krancis Kiwanga wakati wa kusaini Ruzuku kwa ajili ya kusaidia AZAKI za hapa nchini.
No comments:
Post a Comment