HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, October 8, 2018

MAKATIBU WAKUU WA WIZARA 11 WAWASILI MBARALI KUTAFUTA SULUHU YA GN 28 YA MWAKA 2008

NA MWANDISHI WETU.
Makatibu Wakuu kutoka Wizara zinazohusika na suala la Hifadhi ya rasilimali maji na maliasili wamewasili Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya kuanzia Oktoba 4 hadi 6, 2018 ikiwa ni ziara ya kikazi kwa ajili ya kutafuta suluhu ya mgogoro wa mpaka wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha (RUNAPA) na vijiji vya Wilaya ya Mbarali.

Makatibu wakuu hao ni kutoka Wizara mbalimbali zikiwemo; Ofisi ya Rais TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Nishati, Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, na Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Lengo la ziara hiyo ni Kuona na kujiridhisha mambo ambayo yanalalamikiwa kuhusiana na tangazo la Serikali namba 28 la mwaka 2008 (GN. 28 ya 2008.), kupata suruhu ya kudumu ya uchepushaji wa maji katika mto Ruaha pamoja uharibifu wa mazingira katika vyanzo vya mito na mito.

Maeneo yaliyotembelewa na Makatibu Wakuu hao ni pamoja na eneo chepechepe la Ihefu lililopo ndani ya hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Mashamba ya mpunga ya madibira (MAMCOS), Banio la maji lililopo eneo la Mnazi kijiji cha Warumba kata ya Ubaruku pamoja na mashamba ya Mpunga ya mnazi katika kijiji cha Mwanavala Kata ya Imalilosongwe.

Ziara hiyo iliongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera na Uratibu Prof. Faustin Kamuzora na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Albert Chalamila pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe. Reuben Mfune.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof.Faustin Kamuzora akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa Kikao kazi cha Makatibu wakuu wa Wizara zinazohusika na suala la Hifadhi ya rasilimali maji na maliasili walipokutana Wilayani Mbarali mkoani Mbeya kwa ajili ya kutembelea maeneo ya shamba la Madibira, Eneo la Ikolojia ya Tindiga la Ihefu na eneo la hifadhi ya Taifa ya Ruaha tarehe O5 Oktoba, 2018.
 Baadhi ya Makatibu wakuu wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof.Faustin Kamuzora (hayupo pichani) walipohudhuria Kikao kazi hicho.
 Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Dkt.Hamisi Mwinyimvua akichangia hoja wakati wa kikao kazi hicho.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Elisante Ole Gabriel akisisitiza jambo wakati wa kikao kazi cha Makatibu Wakuu walipokutana Wilayani Mbarali ili kutembelea  shamba la Madibira, Eneo la Ikolojia ya Tindiga la Ihefu na eneo la hifadhi ya Taifa ya Ruaha tarehe O5 Oktoba, 2018 Mkoani Mbeya.
 Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Bi.Mariam Mtunguja akichangia hoja wakati wa kikao kazi hicho.
 Baadhi ya Makatibu Mkuu kutoka Wizara mbalimbali pamoja na Mkoa wa Mbeya Mhe.Albert Chalamila (mwenye fulana nyeusi) wakipokea maelezo kutoka kwa Mwikolojia Hifadhi ya Taifa ya Ruaha Dkt.Halima Kiwango walipotembelea eneo la Ikolojia ya Tindiga la Ihefu Wilayani Mbarali Mbeya.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof.Faustin Kamuzora akioneshwa maeneo ya Shamba la Madibira na Mhifadhi kutoka TANAPA Bw.Moronda lililopo katika Kijiji cha Mahango Wilayani Mbarali Mbeya.
 Baadhi ya Makatibu Wakuu wa Watendaji wa Serikali wakipokea taarifa ya Shamba la Madibira kutoka kwa Mwenyekiti wa MAMCOS L.t.d Bw. Stanford Kisinga walipotembelea eneo hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe.Reuben Mfune akifafanua jambo kwa Baadhi ya Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali waliotembelea eneo la shamba la Madibira lililopo Kijiji cha Mahango Mbarali Mbeya.

 (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad