HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 27, 2018

IGP SIRRO AKAGUA UJENZI WA NYUMBA ZA KISASA ZA KUISHI ASKARI NA FAMILIA ZAO MKOANI GEITA

Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Mhe Hamim Gwiyama (aliyesimama) akitoa neno mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, wakati alipofanya ziara ya kikazi katika wilaya hiyo iliyopo mkoani Geita leo 26/10/2018 kwa lengo la kukagua utendaji kazi wa Jeshi la Polisi na utolewaji wa huduma za kipolisi kwa wananchi, wengine ni wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani humo. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akitoka kukagua nyumba  za makazi ya askari zitakazokuwa na uwezo wa kuchukua familia saba za askari wa jeshi hilo zilizopo wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita, zinazojengwa na Watumishi House. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akitoka kukagua ujenzi wa nyumba zinazojengwa kwa ushirikiano wa wafayabiashara na wananchi wa Geita Mjini mkoani Geita leo 26/10/2018 ambapo jumla ya nyumba 20 zitakazokuwa na uwezo wa kuchukua familia 40 za askari Polisi zilizopo katika eneo la Magugu. 
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akimsikiliza kamanda wa Polisi mkoa wa Geita SACP Mponjoli Mwabulambo, wakati akimuonyesha moja kati ya eneo litakalotumika kujenga Ofisi za Makao makuu ya Polisi mkoani humo katika eneo la Magugu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad