Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Andrew
Chenge akiongoza kikao cha sita cha mkutano wa kumi na mbili cha Bunge
hilo leo Jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde, akijibu maswali Bungeni, jijini Dodoma, Septemba 11, 2018.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe.Dkt Hussein Mwinyi
akieleza mipango mbalimbali ya jeshi la kujenga Taifa katika kuanzisha
mafunzo ya stadi za kazi kwa Vijana waliojiunga na jeshi ilo kwa
kujitolea ili waweze kuajiriwa na taasisi zingine za Serikali,Sekta
binafsi au kujiajiri wenyewe.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama, akizungumza Bungeni jijini Dodoma, Septemba 11, 2018.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dkt Philip Mpango akisoma Muswada wa
Sheria ya marekebisho ya sheria ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta
binafsi wa mwaka 2018 leo Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Mhandisi Isack Kamwelwe
akitolea ufafanuzi juu ya changamoto za kivuko cha Mv Mafanikio katika
kusaidia dharura zinazojitokeza kwa wagonjwa hasa akina mama wajawazito
kuhudumiwa wakati wa usiku leo Bungeni Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe.Mhandisi Stella
manyanya akielezea mipango mbalimbali ya Serikali katika kufanikisha
azma nzuri ya uchumi wa Viwanda nchini leo Bungeni Jijini Dodoma.
Mwalimu Joyce Solomon wa Shule ya Tumaini Mission kutoka Arumeru
akifuatilia shughuli mbalimbali za Bunge pamoja na wanafunzi wa shule
hiyo leo Jijini Dodoma.
Picha na Daudi Manongi,MAELEZO.
No comments:
Post a Comment