HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 28, 2018

TASWIRA MBALIMBALI KATIKA SHEREHE ZA KUMUAGA KAMISHNA JENERALI MSTAAFU WA MAGEREZA, DKT. JUMA ALI MALEWA, UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM

Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Alli Malewa akiwa kwenye gari maalum akipita katikati ya Gwaride likiwa katika umbo la OMEGA ikiwa ni ishara ya kumuaga rasmi baada ya kustaafu utumishi wake Jeshini tangu Julai 1, 2018. Hafla hiyo imefanyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam leo Septemba 28, 2018.
Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Alli Malewa akiwasili katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam leo Septemba 28, 2018 kwenye Sherehe za kumuaga rasmi baada ya kustaafu utumishi wake Jeshi tangu julai 1, 2018.
Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akipokea salaam ya heshima kutoka kwa Gwaride maalum lililoandaliwa kwa ajili yake katika Sherehe za kumuaga zilizoandaliwa kwenye Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam leo Septemba 28, 2018.
Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akikagua Gwaride maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza kwa ajili ya kumuaga.
Kikosi cha bendera kikipita mbele ya jukwaa kwa mwendo wa pole.
Gadi ya wanaume iliyoundwa na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza wakipita mbele ya jukwaa kwa mwendo wa pole.
Gadi ya wanawake iliyoundwa na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza wakipita mbele ya jukwaa kwa mwendo wa haraka.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, CGP – Phaustine Kasike akiwa na baadhi ya Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Wageni mbalimbali waliofika katika Sherehe hizo. Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye na katikati ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala.
Askari wa vyeo mbalimbali wakipunga mikono ikiwa ni ishara ya kumuaga na kumtakia kheri Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Alli Malewa(hayupo pichani) katika hafla ya kumuaga iliyofanyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam Septemba 28, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Phaustine Kasike (kulia) akimpongeza Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Malewa mara baada ya gwaride rasmi la kumuaga lililofanyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam.
Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Wakuu wa Magereza Mikoa nchini (wa pili kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.
Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi pamoja na familia ya Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza(Picha zote na Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad