HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 28, 2018

MKUU WA MKOA WA SONGWE AWASIHI WANANCHI KUJITOKEZA KUPIMA AFYA ZAO

Mkuu wa mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemus Mwangela anaawalika wananchi wote katika uzinduzi wa Kampeni ya kitaifa ya kupima VVU na kuanza kutumia ARV ijulikanayo kama "Furaha yangu Pima, Jitambue, Ishi, itakayofanyika kuanza Jumamosi tarehe 29 Septemba 2018, katika eneo la Shule ya Sekondari Nalyelye, Mji ndogo wa Mlowo mkoani Songwe..

Kampeni hii inaendeshwa na mkoa wa Songwe kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia mpango wa kitaifa wa kudhibiti UKIMWI NACP Kwa kushirikiana na shirika la MHRP - HJRMRI.

Kampeni inalenga kuhamasisha wananchi hususan wanaume kupima afya zao. Kwa sasa huduma za upimaji wa afya zinatolewa bure katika iliwa ni upimaji wa VVU, presha, kisukari, uzito na uchangiaji wa damu wa hiyari.

Wote mnakaribishwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad