HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 28, 2018

MFAHAMU DKT. JOSEPH JACKSON, MWAFRIKA ALIYEGUNDUA RIMOTI TELEVISHENI

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
IDADI kubwa ya watu hupenda kuangalia televisheni katika kufuatilia masuala mbalimbali kama vile mpira, muziki na hata tamthiliya, tumekuwa tukitumia kifaa maarufu kama rimoti katika kubadili chaneli mbalimbali Dkt. Joseph N. Jackson ni mwafrika aliyegundua kifaa hicho.

Imeelezwa kuwa kablanya kutokuwepo na kifaa hicho televisheni ilitumika kama rimoti pia hali iliyoleta adha katika kubadilisha chaneli hasa za redio na televisheni.

Jackson alianza kujihusisha na masuala ya ugunduzi  tangu alipokuwa mtoto na katika mahojiano katika vipindi mbalimbali vya redio na televisheni alieleza kuwa akiwa na miaka 8 alifungua redio ili kuweza kuona watu wanaozungumza na hapo ndipo alipoanza kudadisi kuhusiana na teknolojia hiyo.

Akiwa na miaka 17 alikuwa  katika harakati za kutafuta maisha, aliwahi kuhudumu kama msaidizi wa utengenezaji wa vifaa vya mafuta na baadaye alijiunga na jeshi huko Marekani na hii ni kati ya miaka 1956 hadi 1968.

Akiwa anahudumu katika jeshi alianza kuhudhuria shule kwa masomo ya jioni ambako alijifunza namna kufanya matengenezo televisheni na baadaye kumiliki duka lake la matengenezo kwa miaka 7.

Ugunduzi wake wa kwanza ulikuwa ni V chip kifaa ambacho kililenga kufunga maudhui yasiyofaa kwa watoto na hii ilimsaidia sana katika kutengeneza rimoti ambayo imeelezwa aliigundua katika miaka ya 1961.

Dkt. Jackson ni mtoto wa 4 kati ya 8 akiwa na shahada ya uzamivu katika masuala ya fedha na utawala akiwa amehudumu nafasi mbalimbali hasa jeshi kwa miaka 12, uhandisi (nchini Korea) na ametunukiwa tuzo mbalimbali za heshima katika televisheni zikiwemo zilizotolewa na Hollywood na vyuo mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad