HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 6, 2018

KATIBU MKUU WA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO AFUNGUA SEMINA YA UBIA KATI YA SEKTA BINAFSI NA UMMA







Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
KATIBU Mkuu wa wizara ya fedha na mipango, Dotto James amefungua semina ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) cha makatibu wakuu wa taasisi na wakuu wa idara wa wizara ya fedha na mipango inayofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo.

Amesema kuwa semina hiyo itawajengea uwezo maafisa hao kutoka wizara na taasisi wanazooongoza ili waweze kutekeleza miradi ya PPP-(Public service Private partnership) yenye sifa.

James ametoa wito kwa washiriki wa semina wawe na utayari,uzalendo wad hat katika kuchangia, kuchambua kikamilifu miradi yenye sifa ili kuongeza ufanisi na wigo wa kutoa huduma za kiuchumi na kijamii.

“Matumaini yangu kuwa kila mmoja atashiriki kikamilifu katika semina hii muhimu na kupata uelewa wa mambo mhimu yatakayowezesha kuongeza jitihada za maandalizi ya mradi wa PPP.”Amesema James.

Nae Kaimu Mkurugezi wa mkondo wa chini wa shirika la mafuta na gesi (PTDC), Emmanuel Gilbert mradi wa PPP unatambulishwa kwa makatibu wakuu ili serikali na sekta binafsi waweze kushirikiana kikamilifu katika mradi huo.

Amesema kuwa katika uwekezaji katika usambazaji wa mafuta na gesi hapa nchini utasaidia kwa haraka wananchi kuweza kutumia gesi ya hapa nchini.

Amesema kuwa katika mradi huo wa kusambaza gesi utashirikisha waombaji watakao kidhi vigezo kwaajili ya usambazaji wa gesi hiyo ambapo kwa jiji la Dar es Salaam kutakuwa na vituo vitatu ambapo kitakuwa Ilala, Temeke na Kinondoni.
 Katibu Mkuu wizara ya Fedha na Mipango,Dotto James akizungumza  wakati wa kufungua semina ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) cha makatibu wakuu wa taasisi na wakuu wa idara wa wizara ya fedha na mipango inayofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Agosti 6, 2018.
 Mtaalamu wa masuala ya ubia kati ya sekta za umma na sekta binafsi, Philip Kelly  akifafanua jinsi Mradi wa sekta Binafsi na sekta za umma wakati wa semina ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) iliyofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Agosti 6, 2018.
Mtaalamu wa masuala ya ubia kati ya sekta za umma na sekta binafsi, Craig Sugden wakati wa semina ya ubia kati ya sekta ya umma na wakuu wa sekta binafsi (PPP) iliyofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Agosti 6, 2018.
Makatibu wakuu wa taasisi na wakuu wa idara wa wizara ya fedha na mipango wakiwa kwenye semina ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) iliyofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Agosti 6, 2018.

 Makatibu wakuu wa taasisi na wakuu wa idara wa wizara ya fedha na mipango wakiwa kwenye semina ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) iliyofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Agosti 6, 2018 wakimsikiliza Katibu Mkuuwa Wizara ya Fedha, Dotto James(Mbele).




 Makatibu wakuu wa taasisi na wakuu wa idara wa wizara ya fedha na mipango wakifatilia semina ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) iliyofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Agosti 6, 2018.
Kaimu Mkurugezi wa mkondo wa chini wa shirika la mafuta na gesi (PTDC), Emmanuel Gilbert akizungumza na waandishi wa hanbari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya semina ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) iliyofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Agosti 6, 2018.
Picha ya Pamoja ya Makatibu wakuu wa taasisi na wakuu wa idara wa wizara ya fedha na mipango mara baada ya semina ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) iliyofanyika ukumbi wa benki kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Agosti 6, 2018.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad