Na Anitha Jonas – WHUSM,Geita
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amewaahidi wadau wa sekta ya filamu Mkoa wa Geita kufikisha maombi yao ya kupatiwa stika za TRA kwa kazi zao kwa watendaji wakuu wa TRA iliwaweze kupatiwa stika hizo katika ofisi ya TRA za mkoani hapo.
Mheshimiwa Mwakyembe ametoa ahadi hiyo leo mkoani Geita katika kikao na wadau wa kisekta wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo ambapo kikao hicho kililenga la kupata taarifa na kujua changamoto za wadau hao ili serikali iweze kuchukua hatua stahiki.
“Katika sekta ya Filamu nitazungumza na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania ili aweze kufika mkoani hapa na timu yake kwa ajili ya kutoa mafunzo ya namna ya kuandaa miswada ya kazi za filamu kwani changamoto kubwa katika sekta ya filamu ni kuwepo na kazi nyingi zisizo na ubora,”Dkt.Mwakyembe.
Akiendelea kuzungumza na wadau hao Waziri huyo alieleza kuwa serikali kupita idara yake ya Sanaa inaangalia namna ya kutafuta wafadhili watakao toa ufadhili wa kulipia mafunzo ya huduma katika ndege ili washindi wa mashindano ya urembo waweze kupata kazi ya kutoa huduma katika Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).
Pamoja na hayo nae Msemaji Mkuu wa Serikali Tanzania Dkt.Hassan Abbas alitoa elimu ya matumizi ya sheria mbili ambazo ni Sheria ya Haki yakupata taarifa ya mwaka 2016 na Sheria ya Huduma ya Habari ya mwaka 2016,ambapo sheria hizi zinazohusu sekta ya habari na kuwafafanulia waandishi wa habari mipaka yao katika mambo ya kuyatolea habari ikiwemo mambo yanayohusu usalama wa taifa.
“Kwa mwandishi yoyote atakayenyimwa taarifa ambayo niyakutangaza maendeleo ya mkoa huu basi asisite kuniambia kwani sasa ni wakati wa kutangaza maendeleo serikali inayoyafanya ili taifa lijue serikali imetekeleza nini na jitihada zake katika kufanikisha uchumi wa kati zinakwenda vipi.”Dkt.Abbas.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel alieleza kuwa ofisi ya mkoa inashuhughulikia suala la kupatikana kwa eneo la uwanja wa michezo utakao kuwa unatumika kwa ajili ya wanamichezo kufanyia mazoezi na mashindano kwa sasa wakati eneo lililotengwa kwa ajili ya kujengwa uwanja wa kimataifa likiendelea kufanyiwa mchakato wa kufanyiwa ujenzi.
Hata hivyo Mhe. Mwakyembe ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Geita kwa namna unavyotekeleza mikakati yake ya maendeleo na juhudi mbalimbali ambazo wamekisha zifanya katika kuubadilisha mkoa huo na kuwa wa kisasa zaidi.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amewaahidi wadau wa sekta ya filamu Mkoa wa Geita kufikisha maombi yao ya kupatiwa stika za TRA kwa kazi zao kwa watendaji wakuu wa TRA iliwaweze kupatiwa stika hizo katika ofisi ya TRA za mkoani hapo.
Mheshimiwa Mwakyembe ametoa ahadi hiyo leo mkoani Geita katika kikao na wadau wa kisekta wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo ambapo kikao hicho kililenga la kupata taarifa na kujua changamoto za wadau hao ili serikali iweze kuchukua hatua stahiki.
“Katika sekta ya Filamu nitazungumza na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania ili aweze kufika mkoani hapa na timu yake kwa ajili ya kutoa mafunzo ya namna ya kuandaa miswada ya kazi za filamu kwani changamoto kubwa katika sekta ya filamu ni kuwepo na kazi nyingi zisizo na ubora,”Dkt.Mwakyembe.
Akiendelea kuzungumza na wadau hao Waziri huyo alieleza kuwa serikali kupita idara yake ya Sanaa inaangalia namna ya kutafuta wafadhili watakao toa ufadhili wa kulipia mafunzo ya huduma katika ndege ili washindi wa mashindano ya urembo waweze kupata kazi ya kutoa huduma katika Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).
Pamoja na hayo nae Msemaji Mkuu wa Serikali Tanzania Dkt.Hassan Abbas alitoa elimu ya matumizi ya sheria mbili ambazo ni Sheria ya Haki yakupata taarifa ya mwaka 2016 na Sheria ya Huduma ya Habari ya mwaka 2016,ambapo sheria hizi zinazohusu sekta ya habari na kuwafafanulia waandishi wa habari mipaka yao katika mambo ya kuyatolea habari ikiwemo mambo yanayohusu usalama wa taifa.
“Kwa mwandishi yoyote atakayenyimwa taarifa ambayo niyakutangaza maendeleo ya mkoa huu basi asisite kuniambia kwani sasa ni wakati wa kutangaza maendeleo serikali inayoyafanya ili taifa lijue serikali imetekeleza nini na jitihada zake katika kufanikisha uchumi wa kati zinakwenda vipi.”Dkt.Abbas.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel alieleza kuwa ofisi ya mkoa inashuhughulikia suala la kupatikana kwa eneo la uwanja wa michezo utakao kuwa unatumika kwa ajili ya wanamichezo kufanyia mazoezi na mashindano kwa sasa wakati eneo lililotengwa kwa ajili ya kujengwa uwanja wa kimataifa likiendelea kufanyiwa mchakato wa kufanyiwa ujenzi.
Hata hivyo Mhe. Mwakyembe ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Geita kwa namna unavyotekeleza mikakati yake ya maendeleo na juhudi mbalimbali ambazo wamekisha zifanya katika kuubadilisha mkoa huo na kuwa wa kisasa zaidi.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe
(kulia) akizungumza na wadau wa kisekta wa Mkoa wa Geita leo katika
ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo kwa lengo la kupata taarifa za utekelezaji wa
shughuli zao na kujua changamoto zao ili serikali iweze kuchukua hatua
stahiki, kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert
Gabriel.
Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas (kulia) akitoa ufafafuzi wa
sheria mbili zinazohusu sekta ya habari ambazo ni Sheria ya Haki ya
Kupata Taarifa 2016 na Sheria ya Huduma za Habari 2016 leo Mkoani Geita
katika kikao na wadau wakisekta kwa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na
Michezo,kushoto ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Dkt.Harrison Mwakyembe.
Miss Geita 2018 Joyce Magesa akizungumza mbele ya Mhe.Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe leo Mkoani
Geita katika kikao cha wadau wa kisekta kuhusu dhamira yake ya
kushirikiana na serikali kwa lengo la kufanya kazi za kijamii kama Kauli
Mbiu ya Mashindano ya Ulimbwende Duniani mwaka 2018 inavyoelekeza kuwa
ni “Urembo na Kazi kwa Maendeleo ya Jamii” nyuma yake kushoto ni Mkuu wa
Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel.
Wadau wa Michezo Mkoa wa Geita wakiwa katika picha ya pamoja na Mhe.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe
(aliyeketi watatu kushoto) mara baada ya kikao na wadau wa kisekta
kilichofanyika katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Geita leo ,wapili kushoto ni
Mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel na watatu kulia ni Msemaji
Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas.
No comments:
Post a Comment