HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 16, 2018

RICHARD MAYONGELA ATHIBITISHWA RASMI KUWA MKURUGENZI MKUU MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
ALIELYEKUWA Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Tanzania Richard Mayongela athibitishwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini.

Taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habar imesema kuwa amethibitishwa kwenye nafasi hiyo  na Kaimu Mkurugenzi wa Railimali na Utawala  Lawrance Thobias wakati wa Mkutano wa Mameneja wa viwanja vya mikoani na Wakuu wa Vitengo mbalimbali vya Mamlaka.

Amefafanua kwa kueleza kwamba  amethibitisha kupokea barua ya uthibitisho huo kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwele mara baada ya kuona Utendaji wake mzuri katika Mamlaka.

Hivyo kuanzia sasa Mayongela ndio Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya viwanja vya ndege nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Tanzania Richard Mayongela

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad