Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison
Mwakyembe(katikati) akitoa maagizo kwa Maafisa Utamaduni Mkoa na Wilaya
nchini kukamilisha ukusanyaji wa maoni ya wadau wa Sekta ya Utamaduni
kwa ajili ya kuboresha Sera ya Utamaduni ya Mwaka 1997 katika ufunguzi
wa Mkutano wa Saba wa Umoja wa Machifu uliyofanyika leo katika Kijiji
cha Marangu Mkoani Kilimanjaro,Kushoto ni Mlezi wa Umoja wa Machifu
Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mhe.John Samuel Malecela na kulia ni Kaimu
Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Utamaduni Bi.Lilian Beleko kutoka
Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania Chifu Frank Marrialle (kushoto)
akitoa ahadi ya umoja huo kuwasilisha maoni yao kwa ajili ya kuboresha
Sera ya Utamaduni ya Mwaka 1997 kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na
Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe(hayupo pichani) katika ufunguzi wa
Mkutano wa Saba wa Umoja wa Machifu Tanzania uliyofanyika leo katika
Kijiji cha Marangu Mkoani Kilimanjaro,kulia kwake ni Mlezi wa Umoja wa
Machifu Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mhe.John Samuel Malecela.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe
(kulia) akikabidhi nakala 21 za Sera ya Utamaduni ya Mwaka 1997 kwa
Mlezi wa Umoja wa Machifu Tanzania Waziri Mkuu Mstaafu Mhe.John Samuel
Malecela (kushoto) katika Ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Umoja wa
Machifu Tanzania,uliyofanyika leo katika Kijiji cha Marangu Mkoani
Kilimanjaro kwa ajili ya kugawa kwa Machifu waliyoshiriki Mkutano huo
ili waweze kutoa maoni yao kutokana na mapungufu ya sera hiyo
inayofanyiwa marekebisho.
Chifu Nshoma Hawa wa Ukamba Kahama akieleza changamoto zinazomkumba
katika ikulu yake ambapo ardhi ya himaya yake iliyozikiwa machifu
wenzake kuporwa na kugawiwa kwa wananchi kwa ajili ya kilimo kinyume na
utaratibu wa uhifadhi wa ardhi za makazi ya machifu kwa Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (hayupo pichani)
katika Mkutano wa Saba wa Umoja wa Machifu Tanzania uliyofanyika leo
katika Kijiji cha Marangu Mkoani Kilimanjaro.
Chifu Emmanuel Zulu Gama kutoka kwa Wangoni Songea akimwomba Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe(hayupo pichani)
ofisi yake kushiriki katika Tamasha la Mashujaa waliyopigana Vita ya
Majimaji linalofanyika kila Mwaka Mwezi Februari mkoani Songea,katika
ufunguzi Mkutano wa Saba wa Umoja wa Machifu Tanzania uliyofanyika leo
katika Kijiji cha Marangu Mkoani Kilimanjaro.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe
aliyeketi (watano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya
Machifu wa Tanzania mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Umoja
wa Machifu Tanzania uliyofanyika leo katika Kijiji cha Marangu Mkoani
Kilimanjaro,wanne kulia ni Mlezi wa Umoja wa Machifu Tanzania Waziri
Mkuu Mstaafu Mhe.John Samuel Malecela,na wanne kulia ni Mwenyekiti wa
Umoja wa Machifu Tanzania Chifu Frank Marrialle.
Na Anitha Jonas – WHUSM- Marangu
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe amewataka Maafisa Utamaduni Mkoa na Wilaya kuwahimiza wadau wa Sekta ya Utamaduni kuwasilisha maoni yao ndani ya miezi mitatu.
Mheshimiwa Mwakyembe ametoa kauli hiyo leo katika Kijiji cha Marangu Mkoani Kilimanjaro alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa Saba wa Umoja wa Machifu nchini wenye lengo la kujadili namna ya kuhakikisha umoja huo unasajiliwa kisheria pamoja na kuzungumzia nini kifanyike kutokana na kuwepo na mmomonyoko wa maadili katika jamii kwa kiasi kikubwa.
“Serikali iko katika mchakato wa kufanya maboresho ya Sera ya Utamaduni ya mwaka 1997 ambayo imeonekana kuwa na mapungufu kulingana na hali ilivyosasa,hivyo basi nitoe rai kwenu Machifu kama wadau wakuu wa Sekta ya Utamaduni kutoa maoni yenu kwa haraka kwani yatasaidia kwa asilimia kubwa kuongeza ubora katika sera hii tunayoboresha na hivyo basi hakikisheni mnawasilisha maoni yenu kwa Maafisa Utamaduni ndani ya miezi hiyo,”alisema Mhe.Dkt.Mwakyembe.
Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania Chifu Frank Marrialle alieleza kuwa umoja huo ulianza tangu mwaka 2014 na mpaka sasa unajumla ya wanachama 105 na kupitia umoja huo umekuwa ukisisitiza wajumbe wake kusimamia utunzaji mazingira pamoja usimamazi wa maadili katika jamii kwani machifu ndiyo mhimili wa kulinda utamaduni wa taifa.
“Mbali na Machifu hawa kujitahidi kupigania usimamizi wa maadili katika jamii zao wamekuwa wakikumbwa na changamoto nyingi kwani kwa baadhi ya maeneo wamekuwa wakitolewa maneno ya dharau na kejeli kwa kuwaelezwa kuwa utawala wao umepitwa na hauna maana kwa sasa ombi letu kwa serikali ni kuhakikisha kupitia maoni yetu tutakayowasilisha kwa ajili Sera hii ya Utamaduni inayofanyiwa marekebisho yatiliwe mkazo ili kuonyesha wa nguvu ya machifu kwa jamii,”alisema Marrialle.
Aidha,akiendelea kuzungumza Chifu Marialle alipongeza uongozi wa serikali ya awamu ya tano kwa kusimamia utunzaji wa rasilimali za nchi kwa kuhakikisha hakuna utoroshwaji unaofanyika kwa lengo la taifa kupata faida itakayosaidia kuleta maendeleo nchini.
Pamoja na hayo nae Chifu Nshoma Hawa wa Ukamba - Kahama alitoa ombi lake kwa serikali la kuomba kusaidiwa kutokana na ikulu yake kuvamiwa na wanasiasa na kugaiwa kwa wananchi kwa matumizi ya kilimo kinyume na utaratibu wa himaya hiyo kwani eneo hilo ndipo walipozikwa machifu wote wa ukoo huo.
Halikadhalika nae Mlezi Mteule wa Umoja wa Machifu Tanzania Mheshimiwa Waziri Mkuu Mstaafu Mhe.John Samuel Malecela alieleza kufurahishwa na uteuzi huo na kuahidi kushirikia na Machifu hao katika kuhakikisha Machifu hao wanafanikiwa kuleta maendeleo kwa taifa pamoja na kusimamia hali ya kupambana na mmomonyoko wa maadili uliyopo sasa kutokana na hali ya utandawazi.
No comments:
Post a Comment