HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 30, 2018

TFDA YAWATAKA WALISHAJI HAPA NCHINI (CATERING) KUJISAJILI

Na Agness Francis,blogu ya Jamii.
MAMLAKA ya chakula na dawa (TFDA) imesema utoaji wa huduma katika Mikusanyiko lazima uzingatie sheria pamoja kanuni ili kwepusha mad hara kwa walaji wa chakula katika mikusanyiko.

Mkutano huo ulilenga watoa huduma ya chakula kwenye mikusanyiko hapa nchini na kuwataka kujisajili katika mamlaka hiyo na kufuata sheria ya utoaji wa huduma hiyo ikiwemo na mazingira ya uandaji wa Chakula na kufahamu matakwa ya sheria kuhususiana na utoaji huduma hizo kuboresha mifumo ya biashara wa huduma hiyo pamoja na usalama wa chakula kinachotolewa katika mikusanyiko na hivyo kulinda afya ya walaji.

Hayo aliyasema Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Agnes Kijo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa utoaji wa huduma ya chakula katika Mikusanyiko, amesema kuwa kutokana na mabadiliko ya mtindo wa maisha kumekuwa na ongezeko la uhitaji wa huduma ya chakula katika Misiba, Mikutano,MaofisiHarusi.

Kijo amesema ni muhimu kutambua kuwa utoaji wa huduma ya chakula unapaswa kuzingatia Sheria na kanuni bora za usafiri ili kuhakikisha kuwa chakula kinachoandaliwa ni salama ili kulinda afya ya jamii.

"Uandaaji wa chakuka pasipo kuzingatia matakwa ya sheria na kanuni husababisha uchafuzi wa vimelea vya maradhi na hivyo kuweza kusababisha madhara ya kiafya Kama vile Kuhara,Kuhara Damu,Homa ya Matumbo,pamoja na Kipindupindu"amesema Kijo.

Aidha amesema wadau wamejitokeza kutumia fursa hiyo kutoa huduma ya hiyo ya kulisha kama njia ya kujipatia kipato bila kufata taratibu zozote lakini sasa sheria lazima zifuatwe.

Hata hivyo amesema uchafuzi wa vimelea vya maradhi katika chakula imeendelea kuwa tatizo kwa afya ya jamii hasa katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania. 

Amesema mfumo kwa mujibu wa taarifa za shirika la AF ya Duniani (WHO) za mean 2015,inakadiriwa kuwa milioni 600 duniani (sawa na mtu mmoja Kati ya watu 10) huugua kila mwaka kutokana na kula chakula kisicho salama na kati ya hao watu 420,000 hufariki dunia.

Mmoja wa Wadau wa Utoaji Huduma ya Chakula katika Mikusanyiko wa kampuni ya Love Michael Lee amesema kuwa watafuata sheria za TFDA katika kuwaweka huru katika kufanya biashara hiyo.

Amesema kuna uwepo watoa huduma ya vyakula bila kuwa na ujuzi wala kuwa na vibali maalumu.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Agnes Kijo akizungumza wakati akifungua mkutano wa wadau wa watoa huduma ya Chakula Katika Mikusanyiko uliofanyika Jijini Dar es Salaam. 
(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula wa TFDA Justin Makisi akizungumza kuhusiana na madhumuni ya wadau utoaji huduma katika mkusanyiko ,jijini Dar es Salaam. 

Baadhi ya wadau wa watoa huduma ya Chakula katika Mikusanyiko.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad