HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, August 29, 2018

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ATEMBELEA KISIWA CHA GANA

 Naibu waziri Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe,Lucas Boniphace Magembe wakiwa katika  boti ya kizamani, tayari kwa ajili ya safari ya  kwenda katika kisiwa cha Gana 
 katika ziara yake ya  kanda ya ziwa  ya kuwahamasisha wavuvi ufungaji wa samaki kwa vizimba katika ziwa Victoria.
(picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
 Naibu Waziri wa Mifugo na  Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kisiwa cha Gana wilaya ya  Ukerewe mkoa wa Mwanza ambapo aliwasisitiza polisi pamoja na mgambo wanapoenda kwenye operesheni ya kupambana na  uvuvi haramu wawewanaenda na maafisa uvuvi kwa kuwa wao wanajua zana haramu pamoja samaki wasioruhusiwa kisheria.
 Naibi Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akipanda boti ya kizamani, tayari kwa ajili ya safari ya kuelekea katika kisiwa cha Gana Wilaya ya Ukerewe  kwaajili ya kuhamasisha ufungaji wa samaki kwa vizimba katika Vctoria.
 Wananchi wa kisiwa cha Gana wilaya ya Ukerewe  wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega wapili (kushoto) akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Sengerema,Lucas Magembe (kushoto) wakiwasili katika kisiwa cha Gana.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad