HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 5, 2018

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YANYAKUA TUZO MBILI KWENYE MAONESHO YA SABASABA

  Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Utalii, Jaji Mstaafu, Thomas Mihayo ( wa tano kulia) akiwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Deograsius Mdamu (  wa sita kushoto)  wakiwa na Baadhi ya Waoneshaji wakifurahia ushindi wa Tuzo katika banda la Wizara ya Maliasili na Utalii. Tuzo hizo ni mshindi wa kwanza katika kipengele maalum cha Best Export Products Exhibitors na Mshindi wa pili katika kipengele cha Trade in Services  katika Maonesho hayo. Tuzo hizo zilikabidhiwa jana na Waziri Mkuu wa Jahuri ya Muungano wa Tanzania. Majaliwa Kassim Majaliwa katika viwanja vya Sabasaba. ( Picha na Lusungu Helela-MNRT)
 Baadhi ya Waoneshaji wakifurahi ushindi wa Tuzo walizokabidhiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaliwa Kassimu Majaliwa  katika banda la Wizara ya Maliasili na Utalii, Wa kwanza kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Deograsius Mdamu.
 Muonekano mpya wa Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii sehemu ya mapokezi katika Maonesho ya 42 ya  Biashara ya Kimtaifa ya Dar es Salaam .Banda la Wizara limekuwa miongoni mwa mabanda yenye mvuto wa kipekee kutokana na utofauti wake  wa uwepo wa wanyamapori hai kama vile Simba, Chui , Chatu, Nyati, ndege wa aina mbalimbali na wale watakaopenda kuona wanyamapori hao kiingilio ni shilingi 1,000 kwa watu wazima na    500 kwa watoto wadogo. ( Picha na Lusungu Helela-MNRT)
 aswira za  tuzo hizo
 Baadhi ya Waoneshaji wakifurahi ushindi wa Tuzo walizokabidhiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaliwa Kassimu Majaliwa  katika banda la Wizara ya Maliasili na Utalii.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad