WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haina mpango wa kununua madeni yaliyosababishwa na mikopo ya kibenki kwenye vyama vikuu vya ushirika nchini.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Julai 7, 2018) wakati akizungumza na wanaushirika na mamia ya wakazi wa Jiji la Mwanza waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha, jijini humo.
“Serikali ya awamu ya tano hatuna biashara ya kununua madeni ya vyama vikuu, kulikuwa na tabia ya watu wa ushirika kukopa na hali ikiwa mbaya wanakimbilia Serikalini. Serikali hii hatuna biashara hiyo,” amesema.
Waziri Mkuu amesema anazo taarifa kwamba Chama Kikuu cha mkoa wa Kagera (KCU) kimekopa fedha Benki ili kiweze kulipa deni la mwaka 2014. “Nimeambiwa KCU wamekopa fedha benki ili kulipa deni la mwaka 2014, hii inaingia akilini kweli? Mnakopa fedha kulipa deni la zamani, ni kwa nini msiwatafute waliosababisha deni na kuwachukulia hatua?,” alihoji.
“Ninyi mlikuwa watu sita ambao mlikubaliana kama viongozi, mlienda kukopa kuzidi uwezo mlionao. Leo hii ni kwa nini serikali ije kulipa wakati mmetumia ninyi?,” aliuliza Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu amesema Serikali ya awamu ya tatno inasisitiza masuala ya ushirika kwa sababu imeamua kuwahudumia wananchi kuanzia ngazi ya chini kuanzia pembejeo, dawa hadi masoko.
“Tunataka tuondoe utaratibu wa chama kikuu kukopa fedha benki ili kikanunue mazao. Vyama vingi vimetengeneza hasara, leo hii vyama vikuu vina madeni. Hii ni kwa sababu mlikopa fedha benki wakati hata hamjui mna kilo ngapi ambazo zimevunwa.
“Fedha mnachukua nyingi na hata ikibaki hamrudishi benki. Riba anadaiwa mkulima kupitia kilo anazouza, deni anapelekewa mkulima na kuanza kukatwa kwa kila kilo. Hatutaki tena utaratibu huu. Kuanzia sasa, AMCO ndiyo itaratibu na kukusanya mazao ya kila mwanachama kwa sababu yenyewe inajua ina wanachama wangapi, wana ekari ngapi na wanatarajia kuvuna kilo ngapi,” amesema.
Amesema ili kuondokana na utaratibu wa vyama vikuu kukopa benki, Serikali imepiga marufuku utaratibu huo na badala yake wanunuzi wataenda kununua mazao kwenye vyama vya msingi kupitia minada na watatakiwa kuwa wameingiza fedha kwenye vyama vya msingi (AMCOS) ndani ya siku tatu.
“Tulishasema mwisho uwe ni msimu huu, yasijirudie tena haya mambo ya kukopa benki. Mnunuzi akipata mnada, ndani ya siku tatu, anatakiwa awe amehamisha fedha kwenda kwenye akaunti ya AMCOS husika,” alisema.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema mfumo wa ushirika bado unakabiliwa na changamoto ya upotoshaji na maewagiza maafisa ushirika wakasimamie suala hilo kwa kutoa taarifa sahihi kwa wakulima.
“Leo hii tunakabiliwa na changamoto kubwa kupitia uuzaji wa mazao kwa mfumo wa stakabadhi za Mazao Ghalani, Kuna watu wanapita wakipotosha kwamba serikali inawakopa wakulima mazao yao.”
“Nendeni mkawaelimishe wakulima kwamba mtu akipeleka mazao yake ghalani siyo kwamba anakuwa tayari ameuza, bali anayaweka pale na kujua ana kilo ngapi, amapewa risiti na kusubiri bei iwe nzuri wakati wanunuzi wakibishana. Hela ikilipwa, anapewa hela yote kulingana na mzigo wake,” alisema.
Siku ya Ushirika Duniani huadhimishwa Jumamosi ya kwanza ya Julai kila mwaka. Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni: “Ushirika kwa ulaji wa uzalishaji endelevu wa bidhaa na huduma.”
Waziri
Mkuu, Kassim Majalawa akizungumza katika Maadhimisho ya siku ya
ushirika dunianiyaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini
Mwanza, Julai 7, 2018.
Waziri
wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba akizungumza wakati alipomkaribisha
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuhutubia katika Maadhimisho ya siku ya
Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha
jijini Mwanza, Julai 7, 2018.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Mwenyekiti wa Shirikisho la
Ushirika nchini, Bibi Renata Mwageni (kushoto) Tuzo ya Rais John Pombe
Magufuli iliyotolewa na Wanaushirika nchini ili kutambua mchango wa
Rais katika kuendeleza sekta ya ushirika na kuinua uchumi wa wananchi
wa Tanzani ya 2018 . Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Maadhimisho
ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa
Furahisha jijini Mwanza Juni 7, 2018. Wapili kushotoi ni Waziri wa
Kilimo, Dkt. Charles Tizeba na kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na
na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack.
Baadhi
ya wananchi waliohudhuria katika Maadhimisho ya Siku ya Ushirika
duniani wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia
kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mizani ya Kielektroniki ya kupima uzito
wa pamba wakati alipotembelea banda la Chama Kikuu cha Ushirika cha
Nyanza katika maonyesho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika
kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018. Wapili
kulia ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba na watatu kulia ni Naibu
Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwaanjelwa.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama pamba iliyostawi vizuri wakati
alipotembelea banda la Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza baada ya
kuhutubia katika maadhimisho ya siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika
kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018. Kushoto
ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab
Telack. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama pamba iliyostawi vizuri wakati
alipotembelea banda la Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza baada ya
kuhutubia katika maadhimisho ya siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika
kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018. Wanne
kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,
Zainab Telack. Wapili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na
kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Magu Khadija Nyembo.(Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama samaki waliokaushwa wakati
alipotembelea banda la Vyma vya Ushirika katika Soko la Kimataifa la
Kirumba – Mwaloni wilayani Ilemela baada ya kuhutubia katika Maadhimisho
ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa
Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa
Mwanza, Zainab Telack na watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba
na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula ambaye pia ni Mbunge wa Ilemela
.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa TANESCO wakati
alipotembelea banda lao katika maonyesho ya siku ya Ushirika duniani
yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa furahisha jijini Mwanza Julai 7,
2018. Wapili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga, Zainab Telack na watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo,
Dkt. Mary Mwanjelwa.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama pamba na mafuta yanayotokana na mbegu
za pamba wakati alipotembelea banda la Ushirika wa wilaya ya Chato
katika monyesho ya Ushirika yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa
Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018,.
Msanii
wa kikundi cha sanaa cha Buyegi, John Riziki akicheza ngoma ya nyoka
katika Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa
kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018. Mgeni rasmi
katika maadhimisho hayo alikuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
No comments:
Post a Comment