HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, July 3, 2018

TRA YAJIKITA ZAIDI KUHUDUMIA WANANCHI KATIKA MAONYESHO YA SABASABA



Afisa Mwandamizi wa Uchambuzi wa Mifumo ya Biashara wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Makao Makuu Bw. Mathias Chanila akimhudumia mwananchi aliyetembelea Banda la TRA katika Maonyesho ya 42 ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Huduma kwa Mlipakodi ambaye pia ni Mratibu wa Maonyesho ya 42 ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba kwa upande wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Honester Ndunguru (kushoto) akiwaelezea Maafisa wa SIDO haki na wajibu wa Mlipakodi kama ilivyoainishwa katika Mkataba wa Huduma na Mlipakodi wakati walipotembelea Banda la TRA kwenye Maonyesho hayo yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Afisa Elimu na Huduma kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Temeke Bw. Paul Maghembe akimhudumia mwananchi aliyetembelea Banda la TRA katika Maonyesho ya 42 ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Afisa wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Temeke Bi. Jacqueline Fairom akimhudumia mwananchi aliyetembelea Banda la TRA katika Maonyesho ya 42 ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad