Na WAMJW, Dar as Salaam
Mamlaka
ya chakula na dawa TFDA imetakiwa kuwa chachu ya uchumi wa viwanda
hususani katika kuzalisha dawa hapa nchini ili kupata matokeo chanya
katika hatua ya kuinua uchumi wa viwanda.
Hayo
yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na
Watoto Ummy Mwalimu wakati wa kukabidhi vyeti vya ithibaki kwa kiwango
cha kimataifa ISO 17025 kwa maabara ya chakula na maikrobailojia za
TFDA.
"TFDA
isiwe kikwazo kwa wawekezaji nchini hususan Viwanda vya kuzalisha dawa
ili kuunga mkono juhudi za Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt.John Magufuli ya kuelekea uchumi wa viwanda"
Aidha,Waziri
Ummy amesema TFDA wanawajibu wa kuwawezesha wafanyabiashara kutoa
bidhaa zao wanazozileta nchini mapema zaidi Mara wanapokuwa
wamejiridhisha na ubora unaokidhi afya za watanzania na kuwapa vibali
mapema.Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na
Dawa (TFDA )Agnes's kijo amesema wanawajibu wa kuimarisha afya za
watanzania na kuimarisha maabara zao kwa viwango vinavyokubalika
kitaifa.
Kijo
amesema vyeti hivyo vya kimataifa ni ishara kubwa inayoonyesha Kuwa
TFDA inafanya kazi katika kudhibiti ubora wa bidhaa hususan vyakula na
dawa ili kujenga afya za wananchi.TFDA imepokea vyeti vya uthibiti kwa
kiwango cha kimataifa kwa maabara ya chakula na daea ambapo wamefanya
vizuri katika upimaji wa vyakula na dawa vinavyoingia na kutoka nchini.
Waziri
wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA
na baadhi ya wadau wa afya hawapo pichani wakati wa upokeaji wa vyeti
vya Ithibati kwa kiwango cha kimataifa iliyofanyika leo jijini Dar es
salaam.(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA Bi. Agness Kijo
akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka hiyo na baadhi ya wadau
wa afya hawapo pichani wakati wa upokeaji wa vyeti vya Ithibati kwa
kiwango cha kimataifa iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wa
kushoto akikata utepe kuashiria kupokea rasmi vyeti vya Ithibati kwa
kiwango cha kimataifa walivyopewa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA
katika hafla ya kupokea vyeti hivyo leo jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
katikati waliokaa akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Maabara wa
Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA wakati wa upokeaji wa vyeti vya
Ithibati kwa kiwango cha kimataifa iliyofanyika leo jijini Dar es
salaam, wa pili kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na
Dawa TFDA Bi. Agness Kijo.(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
Sehemu ya tendaji wa Mamlaka ya chakula na dawa
No comments:
Post a Comment