HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 16, 2018

MAPOKEZI YA KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA MAKAO MAKUU YA JESHI HILO LEO

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike akipokea saluti kutoka kwa Kamishna wa Utawala wa Magereza, Gaston Sanga mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ofisi ya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jijini, Dar es Salaam, leo Julai 16, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akipokea salamu ya heshima kutoka kwa Gwaride maalum lililoandaliwa kwa ajili ya mapokezi yake Makao Makuu ya Jeshi hilo.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akikagua gwaride maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza.
Kamishna Jenerali mstaafu, Dkt. Juma Malewa(suti nyeusi) akimkaribisha Kamishna Jenerali mpya wa Magereza, Phaustine Kasike mara baada ya kumaliza kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa na maofisa na askari wa Jeshi la Magereza.
Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali nchini wakifanya mahojiano maalum na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike mara baada ya mapokezi Makao Makuu ya Jeshi hilo.
Kamishna Jenerali mstaafu wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(suti nyeusi) akifurahia jambo pamoja na Kamishna Jenerali mpya wa Magereza Phaustine Kasike wakiongozana kuelekea katika mazungumzo maalum na Maofisa, askari na watumishi raia wa Jeshi hilo Makao Makuu ya Magereza.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na Maafisa, askari na watumishi raia wa Jeshi hilo.
Maafisa waandamizi wa Jeshi la Magereza, Maafisa, Askari na watumishi raia wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini hotuba ya Kamishna Jenerali mpya wa Jeshi hilo(Picha zote na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Makao Makuu ya Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad