HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 9, 2018

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU MAALUM YA HALMASHAURI KUU YA CCM ZANZIBAR

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo ameongoza kikao Cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar katika ukumbi wa mikutano Afisi Kuu CCM Zanzibar.
Kikao hicho kilichobeba ajenda kuu mbili, ambazo ni Mapendekezo ya Kupiga Kura za maoni katika uchaguzi wa Jimbo la Jang’ombe na Mapendekezo ya Wanachama wa CCM wanao omba kuteuliwa kugombea nafasi ya Uwakilishi jimbo la Jang’ombe.
Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Dkt. Ali Mohammed Shein yupo safarini nje ya nchi hivyo wajumbe walimchagua Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa Mwenyekiti wa muda na kuongoza kikao hicho.

 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kwenye ukumbi wa Afisi Kuu Zanzibar, kushoto ni Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe.Balozi Seif Idd na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdalla Juma Sadalla. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisoma Ilani ya Uchaguzi ya CCM wakati kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kwenye ukumbi wa Afisi Kuu CCM Zanzibar, kushoto ni Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe.Balozi Seif Idd
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdalla Juma Sadalla akisoma ajenda zitakazojadiliwa kwenye Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar. 
 Wajumbe waliohudhuria Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad