HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, June 24, 2018

WASHINDI WA KAMPENI YA MATUMIZI YA "TEMBOCARDVISA" WA BENKI YA CRDB WAUNGANA NA MASHABIKI LUKUKI WA SOKA NCHINI RUSSIA

 Washindi wa Promosheni ya Shuhudia Kombe la Dunia na TemboCardVisa ya Benki ya CRDB, Nuru Nassor Kisome (katikati) na Danford Martin Muyango (wa pili kulia) wakiwa na washabiki wa timu ya Mexico walipokutana kwenye Treni wakati wakielea kwenye Uwanja wa Spartak, jijini Moscow, Urusi kushuhudia mtanange kati ya Ubelgiji na Tunisia. Hawa ni washindi wa waliopatikana kupitia Promisheni hiyo, ambayo inamuwezesha mteja wa Benki ya CRDB anayefanya miamala mingi zaidi kupitia kadi ya TemboCardVisa kila wiki, kujishindia safari ya kushuhudia mechi mbalimbali za fainali hizo. Mpaka sasa washindi wanne tayari wameshahudhuria mechi hizo. Picha zote na Othman Michuzi.
 Meneja Masoko wa Benki ya CRDB, Jadi Ngwale (kulia) akiwa na Washindi wa Promosheni ya Shuhudia Kombe la Dunia na TemboCardVisa ya Benki ya CRDB, Nuru Nassor Kisome (kushoto) na Danford Martin Muyango muda mfupi baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Ubelgiji na Tunisia, uliochezwa kwenye Uwanja wa Spartak, jijini Moscow, Urusi.
 Washindi wa Promosheni ya Shuhudia Kombe la Dunia na TemboCardVisa ya Benki ya CRDB, Nuru Nassor Kisome (kushoto) na Danford Martin Muyango wakifurahi kwa pamoja huku wakionyesha kadi ya "TemboCardVisa" ya Benki ya CRDB iliyofanikisha kuwafikisha nchini Urusi kushuhudia Kombe la Dunia.
 Nuru Nassor Kisome ambaye ni mmoja wa washindi wa Promosheni ya Shuhudia Kombe la Dunia na TemboCardVisa ya Benki ya CRDB akionyesha furaha yake akiwa uwanjani hapo. 
 Muendeshaji Msaidizi wa Libeneke la Michuzi, Othman Michuzi akiwa na Washindi wa Promosheni ya Shuhudia Kombe la Dunia na TemboCardVisa ya Benki ya CRDB, Nuru Nassor Kisome na Danford Martin Muyango pamoja na Meneja Masoko wa Benki ya CRDB, Jadi Ngwale.
 Wakiwa nje ya Uwanja wa Spartak, Mjini Moscow.
Baadhi ya wadau kutoka nchini Tanzania wakiwa nje ya Uwanja wa Spartak baada ya kumalizika kwa mechi kati ya Ubelgiji na Tunisia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad