Na Mwandishi wetu
Timu ya soka ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imetwaa kombe la benki ya Standard Chartered baada ya kuitandika kwa mikwaju ya penalti 2-1 timu ya Mwananchi Communications Limited .
Kwa ushindi huo, timu ya TBL sasa itakuwa na ziara ya siku 3 nchini Uingereza na kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa ya Standard Chartered yaliyopangwa kufanyika kwenye uwanja wa Anfield, Septemba mwaka huu.
Aidha timu hiyo ya TBL wakifika Anfield wataona mechi ya msimu mpya wa EPL mubashara na kuzungumza na magwiji na kupata nafasi ya kunolewa nao.
Katika michuano hiyo Mchezaji wa Mwananchi, Saidi Seif alifunga mabao manane na kuwa mfungaji bora.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe na gwiji la timu ya Liverpool, Sami Hyypia walishuhudia mechi hiyo na kutoa zawadi kwa washindi.
Akizungumza mara baada ya mashindano hayo kumalizika, Dk Mwakyembe aliipongeza timu ya TBL kwa kutwaa ubingwa na kuishukuru benki ya Standard Chartered kwa kutoa mchango wake kukuza sekta ya michezo.
“Naipongeza benki ya Standard Chartered kwa kuendesha mashindano haya na kuleta hamasa katika soka, nimefarijika sana na nimeshuhudia vipaji vingi, soka ina wigo mpana na ninaamini tunaweza kufanya vyema katika mashindano mbalimbali kwa kutumia vipaji vyetu,” alisema Dk Mwakyembe.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani alisema kuwa benki yao ni wadau wakubwa wa maendeleo ya michezo nchini na katika sekta nyingine na kuahidi kuendelea kufanya hivyo kwa maendeleo ya taifa.
Rughani alisema kuwa wamefarijika sana kuendesha mashindano kutokana na kupata ushirikiano mkubwa kutoka Shirikisho la soka nchini, TFF na serikali.
Katika msimu huu Meneja Uhusiano na Masoko wa benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba amesema kwamba benki yake inafuraha kuendelea kusaidia kukuza vipaji vya vijana nchini kwa kutumia magwiji wa Liverpool.
Alisema benki yake ni wadhamini wa timu hiyo na wamekuwa wakihakikisha kwamba wanashirikiana kukuza vipaji katika nchi ambazo benki inafanyabiashara zake.
Alisema mwaka jana walimleta John Barnes ambaye pia aliendesha kliniki ya soka hali ambayo inaimarisha utaalamu na kisaikoilojia kwa vijana.
Alisema ni lengo la benki hiyo kuhakikisha kwamba wanawalea wataalamu kuboresha vipaji vya soka kukua nchini.
Kukamilika kwa fainali hizo zilizoshirikisha timu 32, pia kunahitimisha ziara ya veteran wa timu ya soka ya Uingereza ya Liverpool, Sami Hyypia ambaye akiwa nchini aliwataka vijana Watanzania kuongeza bidii katika kuhakikisha kwamba wanafikia hatua za juu za uchezaji soka hivyo kupata nafasi ya kucheza Ulaya.
Alisema hayo wakati wa kiliniki ya soka aliyoifanya kwa vijana wa Serengeti boys alipokuwa akishiriki nao katika mafunzo na mazoezi.
Alisema kwamba yeye hakuwa na kipaji kikubwa kuliko alivyoviona kwa vijana hao lakini ameweza kufikia hatua za juu kabisa za uchezaji wa soka kutokana na kujituma kwake.
Alisema amewaambia vijana kuangalia zaidi juhudi kwani kipaji pekee hakitoshi kumfanya mtu kuwa gwiji katika soko.
Alisema pamoja na mafundisho ya walimu ni kazi ya mchezaji mwenyewe kuona udhaifu wake uliopo na kuufanyia kazi ili aweze kuwa mwanasoka bora wa kutregemewa.
Amesema siri kubwa ya mafanikio ni kujituma kwa mchezaji pamoja na kwmaba anakipaji na walimu wazuri.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (wa pili
kulia) akiongozana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered
nchini, Sanjay Rughani (wa pili kushoto), Gwiji la soka, klabu ya
Liverpool, Sami Hyypia (kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Ufundi Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi (kushoto) mara baada ya
kuwasili kwenye mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered
yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (kulia)
akimpongeza Gwiji la soka, klabu ya Liverpool, Sami Hyypia (wa pili
kushoto) kwa kuja nchini kushuhudia mashindano ya kombe la benki ya
Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar
es Salaam. Wengine katika picha ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya
Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani (wa pili kulia) pamoja na
Mkurugenzi wa Ufundi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum
Madadi (kushoto).
Kapteni
wa timu ya kampuni ya Mwananchi Communications Limited, Majuto Omary
(katikati) akimtambulisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,
Dk Harrison Mwakyembe (kushoto) kwa kikosi cha timu hiyo wakati wa
fainali kati ya TBL na MCL katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es
Salaam.
Kapteni
wa timu ya kampuni ya TBL akimtambulisha Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe kwa kikosi hicho baada ya
kutinga fainali za mashindano ya kombe la Standard Chartered
yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani
akisalimiana na kikosi cha timu ya TBL kabla ya kukipiga kwenye fainali
za mashindano ya kombe la Standard Chartered yaliyofanyika katika
viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Gwiji
la soka, klabu ya Liverpool, Sami Hyypia akisalimiana na kikosi cha
timu ya kampuni ya TBL kabla ya kuanza mchezo wa fainali na timu ya
Mwananchi Communications Limited wakati wa mashindano ya kombe la
Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar
es Salaam.
Mgeni
rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison
Mwakyembe, Gwiji la soka, klabu ya Liverpool, Sami Hyypia, Mkurugenzi wa
Ufundi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi pamoja
na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay
Rughani katika picha ya pamoja na timu zilizotinga fainali mashindano ya
kombe la benki ya Standard Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya
Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Wachezaji
wa timu ya TBL (kijani) na Mwananchi Communications Limites (nyeupe)
wakimenyana katika fainali za mashindano ya kombe la benki ya Standard
Chartered yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es
Salaam.
Wadau
kutoka makampuni mbalimbali wakitazama mechi ya timu zilizoingia
fainali kwenye mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered
yaliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Timu
ya soka ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ikisherehekea ubingwa wa kombe
la benki ya Standard Chartered baada ya kuitandika kwa mikwaju ya
penalti 2-1 timu ya Mwananchi Communications Limited katika mashindano
yaliyofanyika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Kapteni
wa timu ya kampuni ya Mwananchi Communications Limited, Majuto Omary
akisalimiana na Gwiji la soka, klabu ya Liverpool, Sami Hyypia wakati
akielekea kukabidhiwa medali na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo, Dk Harrison Mwakyembe katika mashindano ya kombe la benki ya
Standard Chartered yaliyofanyika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es
Salaam.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe
akiwavalisha medali kikosi cha kampuni ya TBL baada ya kuibuka mabingwa
wa mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered yaliyofanyika
viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Mgeni
rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison
Mwakyembe na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini,
Sanjay Rughani kwa pamoja wakikabidhi kombe kwa kapteni wa kampuni ya
TBL mara baada ya kutwaa ubingwa wakombe la benki ya Standard Chartered
baada ya kuitandika kwa mikwaju ya penalti 2-1 timu ya Mwananchi
Communications Limited katika mashindano yaliyofanyika viwanja vya
Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Mabingwa
wa mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered kampuni ya Bia ya
TBL wakishangilia mara baada ya kukabidhiwa kombe hilo wakati
mashindano hayo yalipofikia tamati mwishoni wa wiki katika viwanja vya
Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Mabingwa
wa mashindano ya kombe la benki ya Standard Chartered kampuni ya Bia ya
TBL wakifurahia na kubusu kombe lao mara baada ya kuibuka mabingwa
mashindano ya kombe la Standard Chartered 2018 yalipofikia tamati
mwishoni wa wiki katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Mgeni
rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison
Mwakyembe na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini,
Sanjay Rughani, Gwiji la soka, klabu ya Liverpool, Sami Hyypia pamoja na
Mkurugenzi wa Ufundi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum
Madadi wakiwa kwenye picha ya pamoja na mabingwa wa kombe la Standard
Chartered 2018 yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya
Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani
akiteta jambo na Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard
Chartered nchini, Juanita Mramba mara baada ya kumalizika kwa mashindano
hayo katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe
akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kumaliza zoezi la
kukabidhi kombe kwa mabingwa wa mashindano ya kombe la Standard
Chartered 2018 yaliyomalika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya
Gymkhana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Gwiji la soka, klabu ya
Liverpool, Sami Hyypia.
Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini, Sanjay Rughani
akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa
mashindano ya kombe la Standard Chartered 2018 viwanja vya Gymkhana
jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment