HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 29, 2018

Shangwe za M-Pesa zahamia Jijini Mbeya, gari ya pili yaenda Tukuyu

 Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Paul Ntinika (kushoto) akimkabidhi namba ya gari mshindi wa Mpesa Mkazi wa Tukuyu Wilaya ya Rungwe, Mbeya, Tumaini Msosi (kulia) jana baada ya kuibuka mshindi katika shindano ya mtumiaji bora wa Mpesa kutoka Vodacom wakati wa sherehe za Mpesa kutimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake ambazo zilifanyikia Jijini Mbeya. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Mpesa kutoka Vodacom Tanzania, Ashutosh Tiwaryg.
 Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Paul Ntinika (katikati) akionesha funguo ya gari kabla ya kukambidhi wa mshindi wa gari hilo kutoka Mpesa katika sherehe ya kutimiza miaka 10 ya Mpesa tangu kuanzishwa kwake iliyofanyika jana jijini Mbeya.
Mshindi wa gari kutoka promosheni ya 'Tumia Mpesa ushinde gari', Mkazi wa Tukuyu Wilayani Rungwe, Mbeya, Tumaini Msosi(kulia) akionesha funguo ya gari mara baada ya kukabidhiwa zawadi yake ya gari. Kushoto ni  Mkurugenzi wa M-Commerce kutoka Vodacom Tanzania, Ashutosh Tiwary na katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Paul Ntinika.
 Mkurugenzi wa M-Commerce kutoka Vodacom Tanzania, Ashutosh Tiwary (kushoto) akimpa mkono wa pongezi mshindi wa gari kutoka promosheni ya 'Tumia Mpesa ushinde gari', Mkazi wa Tukuyu Wilayani Rungwe, Mbeya, Tumaini Msosi baada ya kukabidhiwa gari hilo juzi mchana wakati wa hafla ya kusherekea miaka 10 ya Mpesa tangu kuanzishwa kwake.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad