HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 29, 2018

Kazi ya kiongozi ni kujua matatizo ya wananchi- Diwani Nuru Awadh

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Diwani wa Viti Maalum wa Manispaa ya Ilala , Nuru Awadh amesema kuwa kazi ya kiongozi ni kujua matatizo ya wananchi na sio kujifungia kwa kizingizio uchaguzi ulishapita huku wanancho wakiwa na kero ambazo zinakosa majibu kutoka kwa watendaji.

Diwani huyo ameyasema hayo wakati mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Buguruni, amesema kuwa masuala yaliyoibuka kutoka kwa wananchi kuhusiana na uzoaji taka na sungusungu kuwanyanyasa wananchi kuhakikisha yanapatiwa ufumbuzi.

Amesema kuwa wananchi wanakabiliwa na changamoto lakini bila ya watendaji kushughulikia yanafanya wananchi kukosa sehemu ya kusemea kutokana na viongozi kutoitisha mikutano ya hadhara ya kujua matatizo ya wananchi.

Awadh amesema kuwa seriikali inatambua watu wenye ulemavu akiwa nay eye kuwa mwenye ulemavu wa kuona hivyo kwa watu wenye ulemavu katika kata hiyo waendelee kuwa na imani na serikali kutokana n mipango iliyowekwa kwao.

Nae Diwani wa Kata ya Buguruni, Adam Fugame amesema kuwa diwani wa viti maalum amekuwa na udhubutu kwa kuamua kufanya mkutano wa hadhara wa wananchi.

Amesema kuwa matatizo yaliyoibuka watendaji wafuatilie na kupata ufumbuzi ili kuwafanya wanachi kuondokana na  kero.
 Diwani wa Viti Maalum wa Manispaa ya Ilala, Nuru Awadh akizungumza katika Mkutano wa hadhara aliouandaa kwa ajili ya kusikiliza changamoto za wananchi wa kata ya Buguruni uliofanyika katika ofisi ya Mtendaji wa Kata hiyo.
 Diwani wa Kata  ya Buguruni, Adam Fugame akizungumza na wananchi wa Buguruni katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi ya Mtendaji wa Kata hiyo.
 Mwananchi wa Kata ya Buguruni, Siasa Ramadhan akiuliza kuhusiana na walemavu kubaguliwa kufanya biashara katika maeneo ya vituo vya daladala.
 Mwananchi wa Kata ya Buguruni, Sijali Salum akiuliza kuhusiana na walemavu kuhusiana na watu kwenda kuchukua taarifa zao lakini hakuna matokeo na taarifa zinazochukuliwa.

Wananchi wakimsikiliz Diwani wa Viti Maalum, Nuru Awadh katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ofisi ya Mtendaji kata ya Buguruni.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad