HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 30, 2018

RITA KUTOA VYETI VYA KUZALIWA NA MSAADA WA KISHERIA SABASABA

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
WAKALA wa usajili, ufilisi na udhamini (RITA) wanatoa  huduma za usajili kwa watoto chini ya miaka mitano na watu wazima kwa kutoa vyeti vya kuzaliwa.

Akizungumza na Michuzi blog Afisa habari wa RITA Jafari Malema ameeleza kuwa wamejipanga katika msimu huu wa sabasaba katika kuhakikisha watoto wanapata hati zao za utambulisho wa kuzaliwa na watu wazima ambao watasaidiwa kwa msaada maalumu.

Jafari ameeleza kuwa watakua wakiwahudumia wananchi wakati wote wa maonesho na amewaomba wazazi kutumia fursa hiyo kwa kuwapa watoto vyeti vya kuzaliwa vinavyotolewa na mamlaka hiyo.

Aidha ameeleza kuwa licha ya kutoa vyeti vya kuzaliwa RITA itatoa msaada wa kisheria hasa katika masuala ya talaka, ndoa, kuasili mtoto (child adoption), ushauri wa mirathi, wosia na namna ya kuandika na kuhifadhi wosia.

Ameeleza kwamba tangu waanze kutoa huduma hiyo changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni udanganyifu wa majina na mahali na amewataka wazazi kukubaliana majina ya watoto kabla ya kufanya usahili huo.

Jafari ameeleza kuwa ili mtoto aweze kupata cheti cha kuzaliwa mzazi awe na tangazo la kizazi kutoka kituo alichozaliwa mtoto, kadi ya kliniki, cheti cha ubatizo au falaki na kwa watu wazima wawe na tangazo la kizazi kama lipo, kadi ya kliniki, cheti cha shule (msingi/ sekondari) au cheti ya falaki au ubatizo.
 Mafisa mbalimbali wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) wakiendelea na kazi ya kuwahudumia wananchi waliotembelea mbanda hilo katika maonesho ya kimataifa yanayo fanyika Sabasaba jijini Dar as Salaam.
 Afisa habari Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Jafari Malema akiwaelekeza wananchi namna ya kujaza fom za cheti cha kuzaliwa leo jijini Dar as Salaam
 Mariam Ling'ande-Afisa msajili msaidizi akiwakabidhi vyeti vyakuzaliwa wananchi walio fika kwenye banda la RITA na kuhudumiwa.
 Afisa habari Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Jafari Malema akizungumza  leo jiji Dar as Salaam na  Michuzi Blog kuhusu kuwahudimia wananchi wakati ote wa maonesho ya sabasaba.
Wananchi wakiwa katika banda la Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kwenye 

1 comment:

  1. msaada mzuri wa faida kwa watu kupata vyeti na msaada wakisheria,,, lakini vipi kwa waliopo mikoani?,,, na inaoneakna kunaweza kukawa na tatizo kubwa kuliko uko

    ReplyDelete

Post Bottom Ad