HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 4, 2018

MATUKIO MBALIMBALI YA SPIKA WA BUNGE JIJINI DODOMA

Wageni Mbali mbali wakiwemo Manaibu Makatibu Wakuu, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Makamishna wa Bajeti na Sera wakisikiliza hotuba ambapo Wizara ya Fedha na Mipango ilikuwa ikiwasilisha Bajeti yake leo Bungeni Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Mbunge wa Babati Vijijini, Mhe. Jitu Son (kulia) leo katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Walimu na Wanafunzi wa Shule ya Mount Everest kutoka Jijini Dar es Salaam, leo katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia)akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari TUSIIME kutoka Jijini Dar es Salaam, leo katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma. Kushoto ni Mbunge wa Segerea, Mhe. Bonnah kaluwa

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad