Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi)
Selemani Jafo ameziagiza halmashauri ambazo zinaendelea na ujenzi wa
mabweni na madarasa kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi wa kudato cha tano
Julai mwaka huu kuongeza kasi ya ujenzi huo ili ziweze kuwapokea
wanafunzi watakaopangwa katika shule hizo.
Waziri
Jafo aliyasema hayo leo mkoani Morogoro alipokuwa akikagua ujenzi wa
shule ya wasichana ya Sokoine Memorial inayojengwa wilayani Mvomero.
Alipokuwa
wilayani humo, Waziri Jafo amemsisitiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Mvomero kuongeza idadi ya mafundi ili kazi hiyo ifanyike kwa kasi pindi
fedha zilizoombwa za umaliziaji sh.millioni 900 kutoka wizara ya elimu
zitakapotolewa.
Katika
ziara hiyo, Jafo aliongozana na Mkuu wa mkoa Morogoro Dk.Steven Kebwe
ambapo miradi mbalimbali ya elimu na afya ilikaguliwa ikijumuisha
Sekondari mpya ya wasichana ya Sokoine Memorial, kituo cha afya Chazi,
Hospitali Teule ya Bwagala , pamoja na sekondari ya Lusanga.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akikagua ujenzi unaoendelea katika Shule ya Sokoine Memorial wilayani Mvomero
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akisisitiza jambo kwa viongozi na watendaji wa mkoa wa Morogoro na wilaya ya Mvomero wakati wa ukaguzi wa sekondari ya sokoine memorial
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akiongea na wananchi katika kituo cha afya Chazi wilayani Mvomero
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa afya wa Hopitali Teule ya Bwagala iliyopo Turiani wilayani Mvomero
Ukaguzi wa nyumba za watumishi ukiendelea katika sekondari ya sokoine memorial.
No comments:
Post a Comment