HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 24, 2018

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WATAALAM WA KUTENGENEZA MABEHEWA NA VICHWA VYA TRENI ZA MWENDOKASI KUTOKA NCHINI CHINA

 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (katikati) akizungumza na wataalam kutoka Kampuni ya Zhuzhou Locomotive ya nchini China inayojishughulisha na utengenezaji wa mabehewa na vichwa vya treni za Mwendokasi, mapema leo Ofisini kwake Jijini Dodoma.
 Mwakilishi katika bara la Afrika wa Kampuni ya Zhuzhou Locomotive ya nchini China inayojishughulisha na utengenezaji wa mabehewa na vichwa vya treni za Mwendokasi Ndg. Manfred Lyoto (wa kwanza kushoto) akimuelezea Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai jinsi kampuni yao inavyofanya kazi walipomtembelea Ofisini kwake Jijini Dodoma.
  Injinia Mwandamizi wa kampuni ya  Zhuzhou Locomotive ya nchini China Ndg. Peng Zhiliang (katikati) akimuonesha Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kulia) mfano wa kichwa cha treni ya mwendokasi wakati walipomtembelea Ofisini kwake Jijini Dodoma. Kushoto ni mwakilishi wa kampuni hiyo barani Afrika Ndg. Manfred Lyoto
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (katikati) katika picha ya pamoja na wataalam kutoka Kampuni ya Zhuzhou Locomotive ya nchini China inayojishughulisha na utengenezaji wa mabehewa na vichwa vya treni za Mwendokasi,  mara baada ya kuzungumza nao mapema leo Ofisini kwake Jijini Dodoma. Wakwanza kulia ni Mhe. Stansalaus Mabula (Mb) ambaye alikuwa mwenyeji wa Wageni hao. PICHA NA BUNGE

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad