HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 3, 2018

MATUKIO MBALIMBALI YA WAZIRI DKT. MWAKYEMBE ALIPOHOTUBIA SIKU UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na wajumbe wa kongamano la maadhimisho ya kilele cha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo mjini Dodoma.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akizindua mpango maalumu wa Kitaifa kuhusu Muelekeo wa Uhuru wa Kujieleza ulioandaliwa na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini Mwa Afrika (MISA TANZANIA) wakati wa kilele cha kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo mjini Dodoma. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA TANZANIA) Bi. Salome Kitomari.
 Mwakilishi wa UNESCO nchini Bw. Jaco Du Toit (kushoto) akimkabidhi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe moja ya machapisho ya Jumuiya hiyo kuhusiana na Uhuru wa Vyombo vya Habari wakati wa kilele cha kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo mjini Dodoma.
 Mwakilishi wa Jumuiya ya Ulaya hapa nchini Bw. Charles Stuart akizungumza na wajumbe (hawapo pichani) wakati wa kongamano la maadhimisho ya kilele cha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo mjini Dodoma.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) Bi. Edda Sanga akizungumza na wajumbe (hawapo pichani) wakati wa kongamano la maadhimisho ya kilele cha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo mjini Dodoma.
 Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Bw. Deodatus Balile akizungumza na wajumbe (hawapo pichani) wakati wa kongamano la maadhimisho ya kilele cha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo mjini Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa habari, viongozi wa taasisi na Mashrika ya Kimataifa yanayojihusisha na masuala ya habari hapa nchini wakati wa kongamano la maadhimisho ya kilele cha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad