HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 24, 2018

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MHE. STEPHEN MASELE (MB) NA MHE. MBONI MHITA (MB)

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati)akizungumza na Mbunge wa Shinyanga mjini Mhe. Stephen Masele ambaye hivi karibuni amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika pamoja na Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini Mhe. Mboni Mhita ambaye pia amechaguliwa kuwa  Rais wa Caucus ya Vijana ya Bunge la Afrika , ofisini kwa Makamu wa Rais , Kilimani Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mbunge wa Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Masele ambaye hivi karibuni amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika, Mheshimiwa Masele  alimshukuru Makamu wa Rais kwa jitihda zake zilizofanikisha ushindi wake.  (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati)akiwa kwenye picha ya pamoja  na Mbunge wa Shinyanga mjini Mhe. Stephen Masele ambaye hivi karibuni amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika pamoja na Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini Mhe. Mboni Mhita ambaye pia amechaguliwa kuwa  Rais wa Caucus ya Vijana ya Bunge la Afrika  wengine pichani ni Mbunge wa Mbozi Magharibi Mhe. David Silinde (kulia) na Mbunge wa Viti Maalum Wanawake Zanzibar Bi. Asha Juma (kushoto) , ofisini kwa Makamu wa Rais , Kilimani Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa mkono wa pongezi Mbunge wa Shinyanga mjini Mhe. Stephen Masele ambaye hivi karibuni amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika, leo Kilimani jijini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati)akimpa mkono wa pongezi Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini Mhe. Mboni Mhita ambaye pia amechaguliwa kuwa  Rais wa Caucus ya Vijana ya Bunge la Afrika , ofisini kwa Makamu wa Rais , Kilimani Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad