HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, May 6, 2018

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAKUNGA DUNIANI YAFANA ZANZIBAR

 Baadhi ya Wauguzi wa Zanzibar walioshirki  maadhimisho ya siku ya Wakunga Duniani wakiwa katika maandamano kuelekea Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani Kikwajuni ambako maadhimisho hayo yalifanyika rasmi ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed.
 Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashind Mohamed akizungumza na wakunga katika maadhimisho ya siku ya Wakunga Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Wawawkilishi la zamani Kikwajuni Mjini Zanzibar.
 Mwenyekiti wa Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar Bi. Amina Abdulkadir Ali akzungumza na wakunga katika maadhisho hayo yaliyofanyika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Zanzibar.
 Mwakilishi kutoka Shirika la Kimataifa linaloshughulika Idadi ya watu (UNFPA) Batula Abdi Hassan akizungumza na wauguzi walioshiriki maadhimisho ya siku ya wakunga Duniani katika Ukumbi wa Baraza la Wawawkilishi la zamani Kikwajuni Mjini Zanzibar.
 Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed akimkabidhi cheti mmoja wa Wauguzi bora Bi. Rose Abdalla ambae ni mkufunzi mwandamizi kutoka Chuo cha Taaluma ya Sayansi za Afya ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar
Wauguzi kutoka vituo mbali mbali vya Afya Zanzibar walioshiriki maadhimisho ya siku ya Wauguzi duniani wakimsikiliza Waziri wa Afya (hayupo pichani) katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani Kikwajuni (PICHA NA ABDALLA OMAR – MAELEZO ZANZIBAR).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad