HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 25, 2018

BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA SH. 240 MIL KUSAIDIA SEHEMU YA UKARABATI WA JENGO LA WAGONJWA WA DHARULA HOSPITALI YA BUGANDO, MWANZA

Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Uendeshaji na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (katikati) akikabidhi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Beki ya CRDB, Dk. Charles Kimei mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni mia mbili na arobanini (240 mil) kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Bungando, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Mhashamu Yuda Thaddeus Ruwa'ichi, kwa ajili ya kusaidia kukamilisha ukarabati na upanuzi wa Jengo la Huduma za wagonjwa wa dharula (Emergency Medicine Department) katika Hospotali ya Rufaa ya Bugando, jijini Mwanza Mei 25, 2018. kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Dkt. Abel Makubi na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Uendeshaji na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka akitoka hotuba kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Beki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, katika hafla fupi ya kukabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni mia mbili na arobanini (240 mil) kwa ajili ya kusaidia kukamilisha ukarabati na upanuzi wa Jengo la Huduma za wagonjwa wa dharula (Emergency Medicine Department) katika Hospotali ya Rufaa ya Bugando, jijini Mwanza Mei 25, 2018.
Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Bungando, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Mhashamu Yuda Thaddeus Ruwa'ichi akizungumza machache wakati akitoa shukrani kwa Uongozi wa Benki ya CRDB, kwa msaada wa shilingi milioni mia mbili na arobanini (240 mil) kwa ajili ya kusaidia kukamilisha ukarabati na upanuzi wa Jengo la Huduma za wagonjwa wa dharula (Emergency Medicine Department) katika Hospotali ya Rufaa ya Bugando, jijini Mwanza Mei 25, 2018.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Dkt. Abel Makubi (kushoto) akimueleza jambo Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Uendeshaji na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (koti jeusi) aliyeambatana na baadhi ya wakurugenzi wa benki hiyo pindi walipotembelea sehemu ya Jengo la Huduma za wagonjwa wa dharula (Emergency Medicine Department) inayofanyiwa ukarabati katika Hospotali ya Rufaa ya Bugando, jijini Mwanza Mei 25, 2018. Wengine pichani ni baadhi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB pamoja na Uongozi wa Hospitali hiyo.







No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad