Na Ripota Wetu, Globu ya jamii
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni
(Unesco) limesema mafunzo ambayo wameyapata mafundi
mitambo kutoka redio za jami 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar
yalete tija na mabadiliko katika kutekeleza majukumu yao kwa
maslahi ya jamii.
Pia limesema matumaini ya Unesco mafunzo hayo yatakuwa
chachu kwa wale ambayo wameyapata lakini ni vema
waliyoyapata nao wakaenda kuwaelimisha wenzao ambao
wamewaacha maofisini na kufanya hivyo itakuwa na tija zaidi na
kuleta mabadiliko kwa haraka na kubwa zaidi wameomba
washiririki wa mafunzo hayo wasiwaangushe.
Akizungumza wakati akifunga mafunzo kwa mafundi mitambo hao
ambayo yamefanyika kwa siku saba Kaimu Mkuu Ofisi ya Mkuu wa
Kitengo cha Elimu Unesco Dar es Salaam Faith Shayo shirika lao
linayo furaha kuona mafundi mitambo hao wamepata elimu
ambayo inaendelea kuwajengea na imani yao watakuwa na
mabadiliko kutokana na kile ambacho wamekipata kwa muda wa
siku saba walipokuwa wakijifunza.
"Waliopata mafunzo hayo wapo 47 na kila mmoja akifanya kazi
kwa kuonesha mabadiliko maana yake itakuwa na tija.Pia mafunzo
yawe chachu ya huko mnakokwenda kwenye redio zenu tunajua
wapo ambao mmewaacha basi nao mkawape elimu ambayo ninyi
mmeipata,"amesema.
Amefafanua siku saba ambazo wamekuwa wakijifunza na baada
ya kumaliza watakuwa na kitu cha kuwabadilisha maana kikubwa
katika maisha ya binadamu ni kuwa na mabadiliko ambayo msingi
wake yatatokana na elimu.
Amesisitiza elimu waliyoipata mafundi mitambo hao ilete
mabadiliko katika kazi zao na kueleza jukumu la Unesco ni kutafuta
fedha kwa wafadhili na kisha kutoa elimu hiyo lakini juhudi zitabaki
kwa mhusika kufanyia kazi alichofundishwa.
"Huwa tunafuatilia baada ya mafunzo je kuna mabiliko yoyote kwa
wahusika lakini la kufurahisha wengi wenu mmeonesha kubadilika
na kuwa na matokeo yenye tija.
"Fursa ya kubadilika iko ndani yetu, sisi tunaweza kutoa fedha ili
mafunzo yanapatikane lakini hatuna uwezo wa kukushika mkono
bali hilo litabaki kuwa ni uwezo wa mtu mwenyewe na siku hizi
kuna lugha ya kujiongeze.Hivyo baada ya mafanzo hayo naamini
mtaendelea kujiongeza kwa kufanya mabadiliko sehemu za
kazi,"amesema.
Ameeleza namna ambavyo Unesco ina matumaini makubwa na
waliopata mafunzo hayo kwani ikiwangalia inawaona walivyo na
ari ya kujituma na kuleta mabadiliko katika majukumu yao baada
ya kuipata elimu hiyo.
Amewaambia kuwa wanaofadhili mafunzo hayo wao
wanachoangalia baada ya elimu hiyo wahusika wamebadilika kwa
kiwango gani na tija gani inayopatikana kupitia wao,hivyo
akatumia nafasi hiyo kuwaomba wafanye kazi kwa weledi na ujuzi
mkubwa na wasiwaangushe.
Kaimu
Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo akizungumza kuhusu
UNESCO inavyoshiriki moja kwa moja kwenye jamii hasa kuzisadia Radio za
kijamii ili kufanya kazi zake kifanisi wakati wa kufunga mafuzo
ya mafundi mitambo kutoka redio jamii 25 zilizopo Tanzania Bara na
Zanzibar yaliyofanyika kwa siku saba katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam. Mafunzo haya ya siku saba yameratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
Kaimu
Mkurugenzi Idara ya Ufundi kutoka TBC, Joseph Kambanga akizungumza
namna TBC ilivyojitolea kuzisaidia Radio za kijamii ili kuimarisha
upatikanaji wa habari na hata kuimarisha mitambo ya urushwaji wa
matangazo kwenye jamii haraka wakati kufunga mafuzo ya mafundi mitambo
kutoka redio jamii 25 zilizopo Tanzania Bara na Zanzibar yaliyofanyika
kwa siku saba katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mratibu
wa Mafunzo kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Rose Mwalongo akisisitiza umoja wa mafundi
mitambo waliopata mafunzo ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea
wakati wa kufunga mafunzo hayo.
Fundi
Mitambo wa Redio Jamii Orkonerei FM, Baraka David Ole Maika akitoa
shukrani kwa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) pamoja na Shirika la utangazaji la
Tanzania(TBC) kwa kuweza kutoa mafunzo kwa mafundi mitambo kutoka redio
jamii 25 yalifanyika kwa Siku saba katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam.
Mratibu
wa Mafunzo kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Rose Mwalongo(wa kwanza kushoto) pamoja
na walimu waliotoa mada mbalimbali katika mafunzo kwa mafundi mitambo
wakiwa kwenye mkutano wa kufunga mafunzo hayo.
Baadhi
ya mafundi mitambo wa radio za kijamii 25 wakifuatilia mada wakati wa
kufunga mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika kwa siku saba katika
ukumbi wa Uwanja wa Taifa na kuratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
Kaimu
Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo (kushoto) akiwakabidhi
vyeti baadhi ya mafundi mitambo kutoka radio za kijamii 25 za hapa
nchini. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ufundi kutoka TBC, Joseph
Kambanga.
Kaimu
Mkurugenzi Idara ya Ufundi kutoka TBC, Joseph Kambanga (kushoto)
akiwakabidhi vyeti vya kuhitimu kwa baadhi ya mafundi mitambo kutoka
radio za kijamii 25 kutoka Tanzania Bara na visiwani.
Kaimu
Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo akiwa kwenye picha ya
pamoja na wahitimu ambao ni mafundi mitambo kutoka radio za kijamii 25
mara baada ya kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku saba.
No comments:
Post a Comment