HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 30, 2018

TANZANIA KUFAIDIKA NA MRADI MAENDELEO YA KIJAMII KUTOKA KOREA KUSINI

 Na Mwandishi Wetu- Dodoma
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inategemea kunufaika na mradi maalum kutoka Shirika la ‘International Youth Fellowship’ lenye makazi yake nchini Korea ya Kusini kuhusu utoaji wa mafunzo ya kuiwezesha jamii kuwa na tabia, fikra na mtazamo  chanya ili kuwa na ari na hamasa ya kufikia mabadiliko ya kweli na endelevu katika kujiletea maendeleo ya jamii yenyewe na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika Kikao kati ya Serikali na Shirika hilo Katibu Mkuu Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga amesema  kuwa Mradi huu ni muhimu sana katika jamii ya watanzania kwani utasaidia kubadilisha fikra za watanzania katika kukuza ari na raghba ya kujiletea maendeleo wenyewe katika maeneno yao.

Bibi Sihaba ameongeza kuwa elimu hii itasaidia kuimarisha fikra chanya kwa watanzania wote kujitambua na kuona kuwa maendeleo ya kweli na endelevu yanatokana na ufahamu, uelewa na utashi wa wananachi waliojitoa kufanya kazi za maendeleo kwa kushirikiana na Serikali yenyewe ili kutatua changamoto zilizopo na hivyo  kujifikia maendeleo jumuishi kwa manufaa ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Aidha, akizungumza wakati akitoa elimu hiyo kwa ujumbe wa Menejimenti ya Idara kuu Maendeleo ya Jamii, Katibu Mkuu wa Shirika la ‘International Youth Fellowship’ Dkt. Hun Mok Lee amesema kuwa mabadiliko ya fikra ni muhimu katika mendeleo ya Taifa lolote na kama Tanzania inataka kuendelea zaidi inabidi ianze kutoa elimu itakayosaidia kuwajenga na kubadili fikra za watoto na vijana kuhusu utashi wao wa kutatua vikwazo na changamoto ili kujiletea maendeleo yao wenyewe.

Dkt. Lee ameongeza kuwa ili kuwa na taifa imara zaidi Serikali haina budi kuwarithisha wananchi elimu itakayowawezesha kuwa tayari wa kubadili mtindo wa maisha yao kwa kuwa na mtazamo mmoja wa kushirikiana pamoja katika  kila jambo ili kuchangia azma ya kufikia maendeleo thabiti ya watu na Taifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii Bw. Patrick Golwike amesema kuwa Mradi huu unaendana kabisa na dhana ya maendeleo ya jamii na utasaidia kuongeza chachu katika kuleta mabadiliko ya fikra za wananchi kuweza kujitoa kwa dhati kushiriki katika shughuli za maendeleo ili kuhakikisha kuwa maisha ya watanzania yanashamiri na uchumi wa Taifa unapaa. 

Katika kutekeleza mpango huu, Wataalam wa Maendeleo ya jamii wataendelea kuraghibisha jamii kubadili tabia zao kutoka katika desturi za uchumi wa vijungu jiko na imani hasi na hivyo kuwa na fikra chanya zinazochochea azma ya kujiletea maendeleo.
  Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga akizungumza na wadau wa kutoka Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini wakati walipofika katika Ofisi za Wizara Jijini Dodoma kuwasilisha Mpango maalum kuhusu Umuhimu wa Elimu ya Mabadiliko ya Fikra na Mitazamo katika Kujiletea Maendeleo.
 Katibu Mkuu  Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini Dkt. Hun Mok Lee (kulia) na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika hilo hapa Tanzania Jeon Hee Young wakitoa mafunzo kwa Menejimenti ya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii kuhusu uzingatiaji wa Elimu ya Mabadiliko ya Fikra na Mitazamo katika Kujiletea Maendeleo Jumuishi.  
 Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Idara kuu Maendeleo ya Jamii wakifuatilia mafunzo maaalum kuhusu uzingatiaji wa Elimu ya Mabadiliko ya Fikra na Mitazamo katika Kujiletea Maendeleo  yaliyowasilishwa na ujumbe kutoka Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini katika ukumbi wa Wizara jijini Dodoma. 
 Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bw. Raphael Nombo akichangia jambo wakati wa kikao kati ya Wizara na wadauwa Maendeleo kutoka Shirika la International Youth Fellowship kutoka Korea Kusini katika ukumbi wa Wizara jijini Dodoma.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii Bw.Patrick Golwike  akichangia jambo wakati wa kikao kati ya Wizara na wadau wa Maendeleo kutoka Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini katika ukumbi wa Wizara jijini Dodoma.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto Bi. Magreth Mussai akichangia jambo wakati wa kikao kati ya Wizara na wadau wa Maendeleo kutoka Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini katika ukumbi wa Wizara jijini Dodoma.
 Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga na Menejimenti yake wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa maendeleo wa Shirika la ‘International Youth Fellowship’ kutoka Korea Kusini mara baada ya kumalizika kwa kikao cha kujadili uzingatiaji wa Elimu ya Mabadiliko ya Fikra na Mitazamo katika kujiletea Maendeleo Jumuishi kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga akifurahia jambo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la International Youth Fellowship kutoka Korea Kusini Bw. Jeon Hee Young mara baada ya kumalizika kwa kikao kilichojadili  uzingatiaji wa Elimu ya Mabadiliko ya Fikra na Mitazamo katika Kujiletea Maendeleo. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad